Jumapili, Aprili 28, 2024
Dar es Salaam. Mbuzi ni miongoni mwa wanyama wa kufugwa Tanzania ambao wanashika nafasi ya pili kwa wingi bara na visiwani .
Tanzania ina mbuzi zaidi ya milioni 19 ambapo milioni 18.94 sawa na asilimia 99.4 ya wanapatikana Tanzania bara na waliobaki sawa na asilimia 0.6 wanapatikana Zanzibar .
Mikoa ya Arusha, Shinyanga, Geita, Mwanza, Simiyu, Tanga, Manyara, Singida, Dodoma na Mara.
Kati ya mbuzi wote waliopo Tanzania, zaidi ya milioni 13 wanapatikana katika mikoa hiyo 10 huku mkoa wa Arusha ukiwa kinara kwa kuwa na mbuzi wengi zaidi Tanzania.