Jumamosi, Mei 18, 2024
Dar es Salaam. Licha ya teknolojia ya habari na mawasiliano kuwa na umuhimu kwa wanafunzi kupata ujuzi na maarifa mapya, shule za msingi za Halmashauri ya Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu zinakabiliwa na upungufu mkubwa wa vifaa vya Tehama.
Hali hiyo inaweza kuwa kikwazo kwa wanafunzi kupata elimu ya Tehama ambayo inahitajika zaidi wakati huu wa mapinduzi ya nne ya viwanda.