Rais Samia kushiriki mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi wa AU nchini Ethiopia

February 14, 2025 11:05 am · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Mkutano huu unatarajiwa kujadili ajenda mbali mbali ikiwemo matumizi ya nishati safi ya kupikia.
  • Kabla ya mkutano huo Rais Samia pia anatarajia kuhudhuria Mkutano wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika leo.

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, anatarajia kufanya ziara ya kikazi jijini Addis Ababa, Ethiopia, kuanzia  leo hadi Februari 16, 2025 kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU).

Taarifa ya Sharifa Nyanga, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu  iliyotolewa Februari 13, 2025 inabainisha kuwa mkutano huo utahusisha uchaguzi wa mwenyekiti mpya wa umoja huo kwa mwaka 2025.

Uchaguzi huo unafanyika ili kumpata mrithi wa Rais wa umoja huo Mohamed Ould Cheikh El Ghazouani kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Mauritania anayemaliza muda wake.

Kwa mujibu wa Katiba ya AU, kila mwaka wakuu hao wa nchi wanatakiwa kufanya uchaguzi wa nafasi ya mwenyekiti wa wa umoja huo ambaye huchaguliwa kutoka miongoni mwa viongozi wa nchi wanachama, kwa msingi wa mzunguko wa kanda za Afrika.

https://twitter.com/ikulumawasliano/status/1890273534452400608

Aidha, viongozi wapya wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika watachaguliwa, wakiwemo Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, na Makamishna sita.

Mbali na uchaguzi, viongozi hao wwatajadili taarifa ya ushiriki wa Umoja wa Afrika kwenye mkutano wa Nchi Tajiri Duniani (G20), Utekelezaji wa Ajenda 2063 ya Umoja wa Afrika na taarifa kuhusu masuala ya mabadiliko ya tabianchi. 

Mkutano huo pia utajadili ajenda kuhusu Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia iliyopendekezwa na nchi ya Tanzania. 

Hata hivyo, kabla ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa AU, Rais Samia pia atahudhuria Mkutano wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika utakaofanyika leo Februari 2025.

Sanjari na hayo mkutano huo unatarajiwa kujadili masuala muhimu yanayolenga kuimarisha juhudi za AU katika kudumisha amani na usalama, pamoja na kujadili mikakati ya kukabiliana na changamoto zinazokabili bara hili.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV