Rais Samia atengua uteuzi Mkuu wa Wilaya Mbarali, wakurugenzi wanne

January 24, 2023 2:51 pm · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni utenguzi wa pili tangu mwaka 2023 uanze.
  • Utenguzi huo ulianza tangu Januari 22.

Dar es salaam. Huenda leo itakuwa siku mbaya kwa wakurugenzi watendaji wanne wa halmashauri na mkuu wa wilaya mmoja baada ya teuzi zao kutenguliwa. 

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amefanya utenguzi wa viongozi watano ngazi ya wilaya akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Ndiza Mfune.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu na Kusainiwa na Mkurugenzi wake Zuhura Yunus leo Januari 24, 2023, utenguzi huo ulianza Januari 22 mwaka huu.

Viongozi wengine waliotenguliwa ni Msongela Nitu Palela aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Michael Augustino Matomora aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Wengine ni Linno Pius Mwageni, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu mkoani Shinyanga pamoja na Sunday Deogratius Ndori aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe.

Huu si utenguzi wa kwanza kwa Rais Samia tangu mwaka 2023 uanze. Itakumbukwa kuwa Januari 5 mwaka huu, Samia alitengua uteuzi wa Diwani Athumani kuwa Katibu wa Ikulu na kumpa nafasi hiyo Mululi Mahendeka.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV