Rais Samia amteua Ummy Mwalimu kuwa mshauri masuala ya afya
- Ni baada ya kukaa nje ya ulingo kwa takribani miezi 22.
Arusha. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Ummy Ally Mwalimu kuwa mshauri wa Rais wa masuala ya afya ya uzazi, mama na mtoto.
Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk Moses Kusiluka iliyotolewa usiku wa Leo Juni 2, 2026 imethibitisha uteuzi wa kiongozi huyo.
Uteuzi wa Ummy unakuja ikiwa takribani miezi 22tangu awekwe kando katika baraza la mawaziri na miezi nane tangu aenguliwe katika kinyanganyiro cha ubunge kupitia Jimbo la Tanga mjini.