Rais Samia akutana na mjumbe wa Waziri Mkuu wa Uingereza
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mjumbe Maalum wa Waziri Mkuu wa Uingereza anayeshugulikia masuala ya Biashara kati ya Tanzania na Uingereza, Lord Walney wa kwanza kulia katika mji wa Glasgow, Scotland Oktoba 31, 2021. Picha| Ikulu.
- Wakutana kuzungumzia masuala ya biashara kati ya nchi hizo mbili.
- Mjumbe huyo akiahidi kushawishi zaidi wafanyabiashara wa Uingereza kuwekeza Tanzania.
Dar es salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumza na mjumbe maalum wa Waziri Mkuu wa Uingereza, Lord John Walney kuhusu masuala ya biashara kati ya Uingereza na Tanzania.
Rais Samia amekutana na Walney Oktoba 31, 2021 kando ya mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mazingira (CO26) Glasgow,Scotland kwa lengo la kujitambulisha huku akiwa na jukumu la kuwa kiungo kati ya nchi hizo mbili katika masuala ya biashara na utalii.
Mjumbe huyo ameweka bayana kuwa kukutana kwake na Rais Samia kumempa fursa ya kujua vipaumbele vya Serikali ya Tanzania ambavyo vitamuwezesha kuwashawishi zaidi wafanyabiashara wa Uingereza kuwekeza katika sekta ya biashara na utalii Tanzania.
Rais Samia ameeleza kuwa Serikali yake ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Uingereza katika kuboresha biashara baina ya nchi hizo mbili.
Uingereza ni moja kati ya nchi zinazoongoza kuwekeza nchini, hivyo kupitia mjumbe huyo kutaongeza fursa zaidi za kibiashara katika kukuza ushirikiano wa uchumi kati ya Tanzania na Uingereza.
Latest