Rais Samia afanya uteuzi PSSF, Tanesco

December 12, 2025 10:32 am · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  •  Fortunatus Makore Magambo na Plasduce Mkeli Mbossa ndio viongozi walioteuliwa.

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi wapya katika taasisi mbili za umma ili kuboresha utendaji kazi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Desemba 11, 2025  na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Bakari Machumu, akirejea taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Moses Kusiluka, Fortunatus Magambo ni miongoni mwa walioteuliwa.

“ Fortunatus Makore Magambo ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF),” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Kabla ya uteuzi huo, Magambo alikuwa Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi katika mfuko huo nafasi aliyoitumikia tangu mwaka 2018.

Uteuzi wa Magambo, unaziba nafasi iliyoachwa wazi na Dk Rhimo Nyansaho ambaye Novemba 10, 2025, aliteuliwa kuwa mbunge na baadaye Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Dk Nyansaho alihudumu katika mfuko huo kuanzia Mei 26, 2025 alipoteuliwa kwa mara ya kwanza, akitokea Benki ya Azania kwa nafasi ya Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara.

Rais Samia pia amemteua Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Plasduce Mkeli Mbossa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).

Mbossa anaenda kurithi mikoba ya Dk Nyansaho ambaye ndiye aliyekuwa ameishikiria nafasi hiyo hadi uteuzi huu ulipofanyika akiwa ameiongoza bodi hiyo kuanzia Desemba mwaka 2023.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV