Rais Samia afanya mabadiliko Baraza la Mawaziri

April 1, 2022 4:43 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Amefanya mabadiliko madogo yaliyohusisha wizara tatu.

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri yaliyohusisha wizara tatu kwa mawaziri wake kubadilishiwa majukumu.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus katika taarifa yake iliyotolewa Machi 31, 2022 amesema katika mabadiliko hayo aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, George Simbachawene amehamishiwa Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Bunge, Sera na Uratibu.

Nafasi ya Simbachawene imechukuliwa na Dk Damas Ndumbaro, aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.

Rais Samia amemteua Balozi Dk Pindi Chana kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii akitokea Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Bunge, Sera na Uratibu.

Taarifa ya Ikulu imeeleza kuwa mabadiliko hayo yaanza mara moja.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV