Polisi Tanzania yamnasa mwanajeshi wa Marekani akiwa na mabomu manne 

November 17, 2025 11:36 am · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Polisi yasema inaendelea kukusanya ushahidi na kumhoji mtuhumiwa.

Dar es Salaam. Jeshi la Polisi nchini limesema limemkamata Charles Onkuri Ongeta, mwenye uraia pacha wa Marekani na Kenya na cheo cha Sajenti katika Jeshi la Marekani, akidaiwa kuingia nchini akiwa na mabomu manne ya kurushwa kwa mkono aina ya CS M68.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Mark Njera tukio hilo limetokea Novemba 16, 2025 majira ya saa 6:00 mchana katika eneo la mpaka la Sirari, wakati mtuhumiwa akijaribu kuingia Tanzania akitokea Kenya kwa kutumia gari aina ya Toyota Landcruiser.

Kwa mujibu wa Njera, silaha hizo ni marufuku kuingizwa nchini kwa mujibu wa sheria za Tanzania.

“Kwa mujibu wa sheria ya umiliki wa silaha, mabomu ya aina hii hayaruhusiwi kabisa kuingizwa nchini. Hata kama angeomba kibali, asingeruhusiwa kuyapitisha,” amefafanua

Jeshi la Polisi limesema, linaendelea kukusanya ushahidi na kumhoji mtuhumiwa kuhusu tuhuma hizo, kabla ya kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV