Polisi kuimarisha ulinzi sikukuu ya Eid

May 2, 2022 12:29 pm · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Lawahakikishia waumini wa dini ya Kiislamu utulivu na amani wakati kisheherekea siku hiyo.

Mwanza. Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama limejipanga vyema katika kuhakikisha sherehe za sikukuu ya Eid al-Fitr zinasheherekewa kwa amani na utulivu.

Taarifa ya Kamanda wa polisi Mkoa wa Mwanza, Ramadhan Ng’anzi kwa vyombo vya Habari leo Mei 2, 2022 imesema ulinzi utaimarishwa kwenye nyumba za ibada ambapo askari watakua wakipita kwa doria za miguu, pikipiki na magari katika maeneo yote ya Jiji na Mkoa wa Mwanza.

Kamanda amewataka wananchi wanapokwenda kwenye nyumba za ibada au kumbi za starehe wasiache nyumba zao bila uangalizi au kuziacha wazi kwani kunaweza kushawishi wezi kuiba.

Kamanda Ng’anzi amewakumbusha wazazi na walezi kuwa pamoja na kusherekea sikukuu hii wasisahau majukumu yao ya kuwa makini na watoto wao kwa kutowaacha peke yao barabarani na katika sehemu za michezo mfano maeneo ya mialo na kwenye bembea.

“Katika sherehe hizo polisi tunapiga marufuku disko toto, vile vile ni marufuku kwa madereva wa vyombo vya moto kuendesha wakiwa wamelewa au mwendo kasi, endapo ikibainika hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi yao,” amesema Kamanda Ng’anzi

Sikukuu ya Eid al-Fitr kwa Tanzania itasheherekewa kesho, huku nchi nyingine ikiwemo Kenya zinasheherekea leo.

Ofisi za Mufti wa Tanzania na Zanzibar zilitoa taarifa jana na kutangaza kuwa mwezi haukuandama, hivyo Sikukuu ya Eid al-Fitr itakuwa Mei 3, 2022.

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...