Jinsi ya kupika mahindi ya nazi, maziwa

July 24, 2024 6:52 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Mahindi mazuri kwa upishi huu ni mateke na sio makavu.
  • Unaweza kuchanganya mbogamboga upendazo au kitoweo ukipendacho.

Mahindi ni miongoni mwa vyakula vyenye mapishi mengi, yanaweza kuliwa yakiwa mabichi baada ya kuchemshwa, kuchomwa, kukaangwa, kupikwa kama kande pamoja na kutumika kutengeneza unga wa ugali.

Ukiachana na mapishi hayo yaliyozoeleka kwenye jamii nyingi hii leo kwenye Jiko Point tunakwenda kutizama pishi jipya la mahindi, ambayo ni mahindi ya kuunga na nazi au maziwa.

Tuingie jikoni

Hatua ya kwanza ni kuchemsha mahindi (unaweza kuchemsha mazima au kwa vipande vidogo vidogo) mpaka uhakikishe yameiva vizuri kwa mahindi machanga unaweza kutumia dakika 15 -20 ukipata mahindi magumu unaweza kutumia dakika 30 – 45

Baada ya hapo katakata kitunguu maji na nyanya vipande vidogo vidogo kisha weka mafuta katika sufuria, yakipata moto tia vitunguu, kaanga kwa dakika 1 mpaka vianze kuwa laini ndio uweke nyanya.

Hatua inayofuata saga karoti tia kwenye mchanganyiko na ukate kate mahindi vipande vitakavyo kuvutia kisha uweke kwenye mchanganyiko, tia chumvi kisha koroga vizuri na uache jikoni kwa dakika tano mpaka 10.

Ukimaliza hatua hiyo tia tui la nazi liache kwa dakika 3 kisha malizia kwa kuweka majani ya kortimili kwa juu na chakula kitakuwa tayari kwa kuliwa.

Vitu vya kuzingatia

Mahindi yanatakiwa ya chemshwe kwanza yawe ni mateke na sio makavu pia unaweza kuchanganya mbogamboga upendazo au kitoweo ukipendacho.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV