Kande za mahindi mabichi: Chakula bora kuimarisha afya yako

July 6, 2022 12:36 pm · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Unaweza kupika kwa kuchanganya na nafaka ikiwemo maharage.
  • Chakula hicho kinasaidia kuupatia nguvu mwili.

Mwanza. Mahindi mabichi ambayo yametoka kuvuna yanaweza kutumika kwa shughuli mbalimbali ikiwemo mapishi.

Unaweza kutumia mahindi kupata chakula kwa kuyachoma, kuyachemsha au kuyamenya na ukapika kama kande zilizochanganywa na nafaka nyingine. 

Leo katika maujanja ya mapishi tunajikita katika uandaaji kande unazoweza kupika kwa kuchanganya na nafaka ikiwemo maharage, choroko au njugu.

Mahitaji
Pukuchua mahindi yako vikombe viwili au kimoja na nusu itategemea na aina ya familia uliyonayo. Pia andaa maharage kikombe kimoja cha chai, nyanya moja, kitunguu maji, kitunguu swaumu kama utapenda na mafuta kidogo ya kupikia kama kijiko kimoja cha chai.

Chemsha maharagwe yako hadi yaive, chemsha na mahindi pembeni nayo yaive kisha.

Baada ya mchakato huo, chukua sufuria lingine pembeni na uanze kuunga chakula chako pendwa upate ladha nzuri.

Weka kitunguu na nyanya kwenye mashine ya kusagia chakula kutengeneza rojo. Endapo hutatumia mashine, unaweza pia kukwangua au kukata vipande vidogo vidogo.

Bandika sufuria la kupikia kwenye moto wa wastani, weka maharage, rojo ya nyanya, kitunguu saumu, mafuta na kikombe kimoja cha maji. Kama mahindi yako siyo malaini sana weka maharagwe na mahindi pamoja. 

Changanya mchanganyiko huo kisha funika na mfuniko, acha iive taratibu kwa moto wa chini kwa dakika 20, endapo maji yatakauka, ongeza maji zaidi, hakikisha kila kitu kimeiva vizuri.

Baada ya maharage na mahindi kuiva vizuri ongeza tui la nazi, pika kwa dakika 5 nyingine ongeza chumvi ili kupata ladha.

Na sasa chakula chetu kitakuwa kimeiva tayari kupelekwa mezani kwa walaji.  Unaweza kutumia kinywaji chochote kwenye mlo wako huo; chai au juisi.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV