Njia mbadala za kupika mboga kwa kutumia mvuke

March 21, 2022 5:01 pm · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Unahitaji sufuria kubwa, chujio na bakuli.
  • Kwa mbogamboga, utahitaji hadi dakika 15 kuivisha.

Huenda unadhani unahitaji sufuria maalumu ili upike mboga na chakula chako kwa kutumia mvuke.

Hapana, wakati mwingine vyombo vya nyumbani vinatosha kabisa kukuwezesha upike mboga zako za majani kwa njia ya mvuke.

Mahitaji

1: Sufuria kubwa.

2: Bakuli lenye kitako kipana.

3: Chujio la bati lisilo na mshikio au chuujio la nazi.

4: Mfuniko unaotosha vizuri kwenye sufuria.

Kazi ianze

Weka maji kwenye sufuria na kisha bandika sufuria jikoni. Kalisha bakuli ndani ya maji hayo na ni vyema bakuli likawa katikati ya sufuria.

Washa moto ili kuruhusu maji yachemke na kisha anza kuandaa mboga yako.

Kwa mboga za majani ambazo zinahitaji chumvi unaweza kutumia njia ya sufuria ndani ya sufuria. Yaani badala ya chujio, tumia sufuria.

Licha ya kuwepo sufuria maalumu za kupika kwa mvuke, unaweza kutumia njia zingine. Picha| Better homes and gardens.

Maji yakichemka, weka mboga unayotaka kupika kwenye chujio na kisha ukalishe chujio hilo kwenye bakuli ndani ya sufuria.

Funika sufuria na unaweza kuweka kitu kizito juu ya mfuniko ili kutokuruhusu kabisa mvuke utoke. 

Kwa njia hii mboga za majani zinahitaji dakika 10 hadi dakika 15. Baada ya hapo funua sufuria na utoe mboga zako. Unaweza kuwa unageuza mara moja moja wakati ukisubiri.

Utake nini tena? JikoPoint ndiyo mambo yote.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV