Ni uzushi: Chanjo ya corona haina virusi vya Ukimwi

July 15, 2020 8:11 am · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Siyo kweli kuwa chanjo ya Corona ina virusi vya Corona.
  • Ukweli ni kuwa wagonjwa wa Ukimwi wanaweza kupata changamoto ya matibabu wakati huu wa janga la Corona.

Dar es Salaam.Habari za uzushi kuhusu ugonjwa wa virusi vya Corona hazina mipaka. Na sasa chanjo ya COVID-19 imeanza kuzushiwa kuwa ina virusi vya Ukimwi.

Uzushi huo unavumishwa katika kipande cha video inayosamba kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo Youtube inayoeleza  kuwa Afrika imegoma kupewa chanjo ya corona inayodhaniwa kuwa ina virusi vya Ukimwi wakati habari hiyo siyo ya kweli.

Video hiyo iliwekwa mtandaoni Julai 6, 2020 ikiwa na maelezo katika lugha ya kiswahili  ikieleza kuwa “Habari hivi punde Afrika yagoma kupewa chanjo ya corona. Chanjo yasadikika kuwa na virusi vya ukimwi.”


Zinazohusiana:


Ukweli ukoje

Timu ya Nukta Fakti imebaini kuwa habari hiyo ni uzushi na haina ukweli wowote.

Ukitazama habari hiyo ambayo ilikuwa ni taarifa ya habari kutoka Indhaa ya Kiswahili ya Shirika la Habari la Uingereza (BBC) ilikuwa inaeleza habari mbalimbali ambapo moja ilikuwa inaeleza kuhusu wagonjwa wa Ukimwi wasiofikiwa ipasavyo kutokana na janga la Corona.

Kimsingi habari hiyo haikuelezea kuhusu chanjo ya Corona kuwa na virusi vya Ukimwi. Kwa hiyo inapaswa kupuuzwa.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV