Necta yatangaza matokeo kidato cha nne 2022, ufaulu waongezeka kiduchu

January 29, 2023 8:19 am · admin
Share
Tweet
Copy Link

Bado idadi ya waliopata ufaulu mzuri wa daraja la I-III unaowapa fursa zaidi ya kuendelea na masomo ya elimu ya juu bado wapo chini ya nusu.


Dar es Salaam. Ubora wa ufaulu katika matokeo ya kidato cha nne mwaka 2022 umeongezeka kiduchu baada ya wanafunzi 456,975, kati ya 520,558 waliofanya mtihani huo kupata madaraja ya I hadi IV kiwango ambacho ni sawa na asilimia 87.8% ya watahiniwa wote.

Kiwango hicho cha ufaulu, kwa mujibu wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), kimeongezeka kwa asilimia 0.49 ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2021 ambapo asilimia 87.30 ya watahiniwa walifaufulu kwa madara la I hadi IV.

Kati ya wanafunzi waliofaulu mtihani huo mwaka 2022, wasichana ni 243,285 sawa na asilimia 87.08 na wavulana ni 213,690 sawa na asilimia 88.6.

Kaimu Katibu Mtendaji wa Necta, Athuman Amas amewaambia wanahabari jijini Dar es Salaam kuwa ufaulu umepanda kwa asilimia 0.49. Picha|Esau Ng’umbi/Nukta. 

Licha ya ufaulu huo kuongezeka kiduchu, bado watahiniwa waliopata daraja la I hadi III bado ni wachache zaidi wasiozidi hata nusu ya watahiniwa wote waliofanya mtihani huo Oktoba mwaka jana.

Kaimu Katibu Mtendaji wa Necta, Athuman Amas amewaambia wanahabari jijini Dar es Salaam leo Januari 29, 2023 kuwa ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliopata watahiniwa wa shule unaonesha watahiniwa waliopata ufaulu mzuri daraja la I hadi III ni 192,348 sawa na asilimia 36.95.

Hii ina maana kuwa ni watahiniwa 37 tu kati ya 100 waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana wamepata ufaulu mzuri unaowapa fursa zaidi ya kuendelea na elimu ya kidato cha tano au kwenda vyuo vya kati vinavyotoa vyeti na astashahada.

“Mwaka 2021 watahiniwa waliopata ufaulu mzuri kama huo walikuwa 173,422 sawa na asilimia 35.84 hivyo ubora wa ufaulu umeongezeka kwa asilimia 1.11,” amesema Amas.

Kupata matokeo bonyeza hapa

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV