Ndege ya Precision Air yaanguka ziwani, Rais Samia akiwaomba Watanzania utulivu

November 6, 2022 8:46 am · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link
  • Rais Samia Suluhu Hassan awasihi Watanzania kuwa na utulivu wakati vikozi vya ukoaji vikiendelea kuwaokoa waliohusika katika ajali hiyo.

Dar es Salaam. Ndege ya Shirika la Ndege la Precision Air imeanguka kwenye Ziwa Victoria baada ya kukumbukwa na hali mbaya ya hewa wakati wa kutua katika uwanja wa ndege wa Bukoba huku Rais Samia Suluhu Hassan akiwataka Watanzania kuwa watulivu wakati uokoaji ukiendelea.

Taarifa za kuanguka kwa ndege hiyo katika ziwa hilo kubwa zaidi barani Afrika zilianza kusambaa mtandaoni mapema asubuhi ya Jumapili, Novemba 6, 2022 majira ya Saa 3 kabla ya mamlaka kuthibitisha ajali hiyo.

Precision Air imesema ndege hiyo namba PW 494 iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam ilipata ajali wakati ikianza kutua katika uwanja huo uliopo kandokando mwa Ziwa Victoria.

“Kikosi cha waokoaji kimepelekwa eneo la ajali na taarifa zaidi tutazitoa baada ya muda wa saa mbili,” kampuni hiyo ya ndege imeeleza katika taarifa yake kwa umma.

Rais Samia amesema amepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali hiyo na kuwatumia salamu za pole watu wote walioathirika na ajali hiyo.

“Tuendelee kuwa watulivu wakati huu zoezi la uokoaji likiendelea huku tukimuomba Mwenyezi Mungu atusaidie,” amesema Rais Samia.

Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) limeeleza kuwa ndege hiyo ilianguka ziwani baada ya kuathiriwa na upepo mkali na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika mkoa wa huo wa Kaskazini Magharibi mwa Tanzania.

TBC imesema kuwa mashuhuda wameeleza kuwa watu zaidi ya 15 wameokolewa na kukimbizwa moja kwa moja katika Hospitali ya Kagera huku vikosi vya uokoaji vikiendelea kuwaokoa wengine waliosalia ndani ya ndege inayoelea ziwani. Hadi sasa idadi ya waliohusika katika ajali hiyo haijawa bayana.

Video zilizochapishwa na TBC zinaonyesha kuwa vikosi vya uokoaji vinaendelea kuokoa huku boti ndogo zikivuta ndege hiyo kuelekea eneo la ufukwe wa Ziwa Victoria.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV