Nchi 10 zilizoongoza kwa uwekezaji (FDI) Tanzania 2024

Uwekezaji wa kigeni nchini Tanzania ulikua kwa asilimia 12.1 katika hisa (stock) mwaka 2024, kwa mujibu wa Ripoti ya Uwekezaji Tanzania 2025, mwenendo unaobainisha imani ya wawezaji wa nje nchini.
Katika mwaka huo, ripoti hiyo inabainisha kuwa uwekezaji wa kigeni pia ulikua kwa asilimia 17.1 kwa fedha zinazoingia nchini (inflows), hatua inasaidia kuingiza fedha za kigeni.
Ripoti hiyo iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) hivi karibuni inabainisha kuwa kiasi cha uwekezaji (FPI) kilifikia Dola za Marekani bilioni 24.75 ambapo asilimia 87.7 ilitokana na uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje (FDI) na asilimia 11.2 kutoka uwekezaji mwingine (OI).
Mafanikio haya yalichangiwa na kuongezeka kwa mtiririko wa FDI, hasa kupitia uwekezaji wa faida zilizorejeshwa (reinvestment of earnings) na mikopo ya muda mrefu kati ya makampuni yanayohusiana.
Kwa upande wa nchi zilizoongoza kuwekeza nchini Tanzania, Uingereza ilisalia kuwa mwekezaji mkuu kwa mwaka wa tatu mfululizo ikimiliki asilimia 26.9 ya hisa zote za uwekezaji.
Mwaka 2023, Uingereza iliwekeza kiasi cha Dola za Marekani bilioni 5.13 za Marekani baada ya kuwekeza Dola bilioni 3.95 mwaka 2022.
Kwa mwaka 2024, kuongezeka kwa uwekezaji kutoka Uingereza kunahusishwa na ununuzi wa hisa zilizokuwa zikimilikiwa na wawekezaji kutoka Canada na visiwa vya Cayman katika sekta ya madini.
Latest