Mzee Mtei afariki dunia, Rais Samia amlilia

January 20, 2026 9:20 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Amefariki dunia usiku wa kuamkia Januari 19, 2025, katika Jiji la Arusha.

Arusha. Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na mmoja wa waasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mzee Edwin Mtei, amefariki dunia usiku wa kuamkia Januari 19, 2025, katika Jiji la Arusha.


Taarifa za kifo hicho zilichapishwa kupitia chapisho lililotolewa katika ukurasa wa mtandao wa kijamii wa X (zamani Twitter) na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John heche ambaye amesema kuwa chama hicho kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba huo.


“Tumepokea taarifa kwamba muasisi wa chama chetu, Mzee Edwin Mtei, amefariki dunia usiku wa leo tarehe 19/01/2025. Chama chetu kitatangaza taarifa rasmi kesho asubuhi,” ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo.


Mzee Edwin Mtei aliwahi kuhudumu kama Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania kwa kipindi cha takribani miaka saba, kuanzia Juni mwaka 1966 hadi Januari 1974, akiacha alama muhimu katika historia ya sekta ya fedha na siasa nchini Tanzania.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV