Mwendo wa kuperuzi: Watumiaji wa intaneti wazidi kuongezeka Tanzania

February 18, 2022 7:51 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Idadi ya Watanzania wanaotumia intaneti imeongezeka hadi kufikia milioni 29.8 mwaka 2021.

Dar es Salaam. Huenda idadi ya Watanzania wanaonufaika na fursa za mtandaoni imeongezeka, baada ya takwimu mpya za mawasiliano kuonyesha kuwa idadi ya Watanzania wanaotumia intaneti imeongezeka hadi kufikia milioni 29.8 mwaka 2021. 

Fursa zinazopatikana mtandaoni ni pamoja na biashara, ujuzi na maarifa yanayohitajika kuboresha maisha. 

Ripoti ya takwimu mpya za robo ya nne ya mwaka 2021 za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zilizotolewa hivi karibuni, zinaonyesha kuwa watumiaji wa intaneti wameongezeka hadi kufikia milioni 29.8 mwaka jana kutoka milioni 28.5 wa mwaka 2020. 

Hata hivyo, ripoti hiyo haijaweka wazi ni aina gani ya intaneti inayotumiwa zaidi na Watanzania kama ambavyo imekuwa ikifanyika miaka iliyopita, ambapo intaneti inayohamishika (mobile wireless) ambayo hutumika zaidi na simu za mkononi, tableti na kompyuta mpakato ndiyo imekuwa ikitumiwa zaidi na Watanzania.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Nukta TV

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

Nukta TV

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV