Mwanza yazuia watoto, wazee kumuaga Magufuli uwanjani

March 23, 2021 8:45 am · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Mkuu wa mkoa asema wanaweza kukaa nyumbani na kufuatilia kwenye runinga.
  • Hatua hiyo huenda ikaepusha wakazi hao na madhara ya msongamano mkubwa.

Mwanza. Zikiwa zimesalia chini ya Saa 24 ili wakazi wa Mwanza wamuage mpendwa wao hayati Rais John Magufuli, Serikali imewazuia wazee na watoto kwenda uwanja wa CCM Kirumba kutoa heshima za mwisho kuwaepusha na madhara yanayoweza kutokea kutokana na msongamano mkubwa.

Wakazi wa Mwanza wanatarajia kuuga mwili wa hayati Rais Magufuli mapema Machi 24 mwaka huu baada ya wenzao wa Zanzibar kufanya hivyo leo.

Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Mwanza John Mongella aliiambia kamati ya maandalizi Machi 22 jioni kuwa shughuli za kuaga mwili wa Rais Magufuli aliyefariki Machi 17 mwaka huu zitafanyika kwa amani na utulivu.

Hatua hiyo huenda ikasaidia kuepusha vifo na majeruhi katika msongamano mkubwa kama vilivyotokea wakati wa kuaga mwili wa kiongozi huyo jijini Dar es Salaam ambapo familia moja imeripotiwa kupoteza ndugu watano wakiwemo watoto wanne.



“Idara zote za ulinzi na usalama zimejipanga kuhakikisha ulinzi na usalama unaimarika, na nitoe ombi kwa wazazi na walezi kuhakikisha watoto wanabaki nyumbani wakitazama kwenye runinga kwa kuwa matangazo yanarushwa kwenye channel (idhaa) zote za ndani,” amesema Mongella ambaye ni mwenyekiti wa maandalizi hayo.  

Mongella, ambaye alifika katika viwanja hivyo kushuhudia maandalizi ya uwanja huo, amesema anajua kuwa Rais Magufuli ni kipenzi cha watu wa Mwanza na Kanda ya Ziwa hivyo wanategemea idadi kubwa ya watu.  

Kuhusu ratiba ya kuaga, amesema mageti ya kuingilia uwanjani yatafunguliwa kuanzia saa 10 usiku na mwili utapokelewa uwanja wa ndege saa 1 asubuhi ukitokea Zanzibar.

Baada ya kupokea uwanja wa ndege, mwili huo wa Rais Magufuli utapelekwa uwanjani moja kwa moja kisha sala, dua na maombezi yatafanyika.

Baadae viongozi mbalimbali wa kitaifa na mkoa watatoa heshima zao za mwisho kisha mwili kuruhusiwa kupitishwa kwenye barabara mbalimbali za mkoa wa Mwanza.

Kwa mujibu wa Mongella,  barabraba ambazo mwili huo utapitishwa ni makongoro,  Pasiansi,  musumbiji, Mwontensori,  Loreto,  Buzuruga,  Babati,  na Mjinj kati. barabara nyingine ni CCM mkoa,  Igogo,  Nyegezi,  mkolani,  Buhongwa,  Usagara,  Kigongo kisha utavuka maji kwenda Sengerema.

Amewaomba wananchi kujitokeza na kuweka na staha kwenye msafara ili kuhakisha mtu yeyote hadhuriki.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Nukta TV

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Nukta TV

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Nukta TV