Mwakyembe azipa somo taasisi za mawasiliano Afrika

May 25, 2019 7:50 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Amesema ni wajibu wa vyombo  vya habari kutumia majukwaa yao kutetea na kutangaza mafanikio yaliyopo Afrika. Picha|Mtandao.


  • Amezitaka zitoe kipaumbele katika kutangaza zaidi maendeleo ya bara hilo.
  • Amezitaka zijitofautishe na vyombo vya habari vya nje vya bara hilo ambavyo amedai vimekuwa vikiripoti zaidi mambo mabaya. 
  • Awakumbusha vijana kufuatilia historia ya Afrika na kuweka mikakati thabiti ya kujikwamua kiuchumi.

Dar es Salaam. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amesema taasisi za habari na mawasiliano barani Afrika zina wajibu kulitangaza bara hilo kwa mambo mema yanayofanyika na “kuachana na propaganda za magharibi”. 

 Dk Mwakyembe aliyekuwa akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Mawasiliano Barani Afrika jijini Dar es Salaam, amesema taasisi hizo hazina budi kuonyesha uthubutu kwa kuweka sera zinazoakisi maendeleo na kuyatangaza kwa wananchi na nje ya bara hilo.

Akizungumzia vyombo vya habari vya Afrika,  amevitaka kujitofautisha na vyombo vya nje ya bara hilo ambavyo amedai vimekuwa vikipotosha na kubeza kwa makusudi mambo mazuri yanayotekelezwa na yaliyotekelezwa na nchi za Afrika.

Amebainisha kuwa maudhui ya vyombo vya habari vilivyopo nje ya bara la Afrika vinavyoongozwa na mataifa makubwa huripoti na kutangaza zaidi mambo mabaya yanayohusu Afrika ikiwemo njaa, magonjwa, vurugu za kisiasa na vita. 


Zinazohusiana:


Amesema ni wajibu wa vyombo  vya habari kutumia majukwaa yao kutetea na kutangaza mafanikio yaliyopo Afrika.

“Wakati Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Kenneth Kaunda wa Zambia walipoamua kujenga reli ya Tazara, walipingwa vikali sana na wakoloni waliotutawala na wengine waliita reli ile kuwa ni bamboo (mianzi) lakini ni taifa moja tu la China walitusaidia na leo hii reli ile ndiyo ndefu zaidi katika bara la Afrika yenye urefu wa kilometa 1,860,” amesema Dk Mwakyembe.

Katika hatua nyingine, Waziri huyo amewataka vijana wa Afrika ikiwemo Tanzania kujifunza historia ya bara lao ili kuweza kufahamu wapi walipotoka na wapi wanapoelekea badala ya kulalamika pasipo kuweka mikakati ya namna bora ya kupiga hatua za kujiletea maendeleo yao ya kijamii na kiuchumi.

Naye Rais wa Chama cha Maafisa Uhusiano wa Sekta Tanzania (PRST), Loth Makuza amesema kuwa taasisi yake kwa kutumia Tehama imeweza kutengeneza majukwaa yanayotangaza masuala mbalimbali ya kimaendeleo yaliyofikiwa katika nchi za Afrika, lengo likiwa ni kubadili mtazamo hasi wa bara la Afrika katika diplomasia ya kimataifa hasa katika nyanja za kiuchumi na kijamii.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV