Jumatatu, Julai 08, 2024
Kwa mujibu wa ripoti ya Dijitali ya Januari 2019 iliyotolewa kampuni ya We are social ya nchini Marekani inaeleza kuwa licha ya changamoto za usiri, udukuzi, habari za uongo na mambo mengine hasi ya maisha ya mtandaoni, bado dunia inaendelea kushikamana na intaneti na mitandao ya kijamii.
Ukuaji wa matumizi ya intaneti duniani hauonyeshi dalili yoyote ya kupungua huku maelfu ya watu wakiingia mtandaoni kila siku. Ukuaji huo ndiyo unaochochea matumizi ya mitandao ya kijamii.