Mpina akwama mahakamani, ndoto za Urais 2025 zayeyuka

October 15, 2025 3:47 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya Mahakama Kuu Masjala Kuu Dodoma kusema Inec haipaswi kuingiliwa na chombo chochote.
  • ACT Wazalendo yasema inakusudia kukata rufaa ikishirikisha wadau wa kimataifa na kitaifa.

Dar es Salaam. Mahakama Kuu Masjala Kuu Dodoma imeitupa kesi ya Luhaga Mpina na ACT-Wazalendo, ikieleza kwa mujibu wa Sheria na Katiba ya nchi, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) haipaswi kuingiliwa na chombo chochote kwa jambo ambalo ilifanya kwa nia njema.

Mpina alikuwa akipinga kuenguliwa katika nafasi ya kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Uamuzi huo umetolewa leo Jumatano Oktoba 15, 2025 mbele ya mahakama hiyo na kiongozi wa jopo la majaji wanaosikiliza kesi hiyo Jaji Fredrick Manyanda. Majaji wengine waliosikiliza kesi hiyo ni Sylvester Kainda na Abdallah Gonzi.

Kwa uamuzi huo, Mpina hataweza kushiriki kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu, ambao kwa sasa vyama vya siasa vinavyoshiriki vinaendelea na kampeni.

Hata hivyo, Chama cha ACT Wazalendo kimetangaza kuchukua hatua za kisheria ikiwemo kukata rufaa ya uamuzi huo.

Taarifa ya Mwanasheria Mkuu wa ACT iliyotolewa muda mchache baada ya hukumu hiyo imebainisha kuwa  sambaba na kukata rufaa ya uamuzi huo  ACT itawashirikisha wadau wa ndani na nje ya nchi ili kuendelea kupigania mabadiliko ya kisheria na kikatiba katika mchakato wa uchaguzi.

Aidha, ACT Wazalendo imewashukuru wanachama na wafuasi wake kwa mshikamano na kujitoa wakati wote wa mashauri hayo na kuwataka kuwa watulivu, wamoja, na kuendelea kujielekeza kwenye mapambano ya demokrasia na haki. 

“Tubaki wamoja na safari inaendelea” imeeleza taarifa hiyo.

Hii ni kesi ya pili kwa Mpina ndani ya mwezi mmoja akipigania haki yake ya kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29. 

Awali Mpina alienda mahakamani kupinga uamuzi wa INEC kumzuia kurejesha fomu za kuwania kiti hicho na Mahakama Kuu ilimpa ushindi. 

Hata hivyo, siku moja baada ya kurejesha fomu na kuteuliwa kuwania Urais, INEC ilimuondoa tena kwenye orodha ya wagombea baada ya kupokea pingamizi kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
17 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Nukta TV

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Nukta TV

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Nukta TV