Mnara wa Eiffel nchini Ufaransa wafungwa kwa muda usiojulikana

May 21, 2019 1:44 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Mnara wa Effeil uliopo Paris, Ufaransa umefungwa kwa muda usiojulikanana. Picha|Mtandao.


  • Umefungwa jana baada mwanaume mmoja kukutwa akipanda juu ya mnara huo bila ruhusa.
  • Watalii waondolewa eneo hilo na washauriwa kusitisha safari za kutembelea mnara huo. 

Mnara wa Eiffel uliopo katika jiji la Paris nchini Ufaransa ambao hutumika kama kituo cha shughuli za utalii umefungwa kwa muda usiojulikana baada ya mwanaume mmoja kukutwa akipanda kuelekea juu ya mnara huo bila ruhusa.

Kwa mujibu wa Shirika la habari la Associated Press, mwanaume huyo alikutwa kiasi cha futi 900 juu ya mnara huo na bado haijajulikana aliwezaje kupenya viunzi vya maafisa wa usalama wanaolinda eneo hilo mpaka kufikia hatua ya kutaka kupanda mpaka juu ya mnara huo. 

Kutokana na kadhia hiyo, watalii takriban 2,500 waliokuwepo katika eneo hilo waliondolewa mara moja na mnara huo umefungwa kwa muda usiojulikana.  Uamuzi wa kuufunga mnara huo ulifikiwa jana (Mei 20, 2019).


Inayohusiana: Haya ndiyo maeneo yanayotembelewa zaidi na watalii duniani


Kampuni inayosimamia mnara huo ya The Eiffel Tower Exploitation Company imewashauri watalii wanaokusudia kutembelea eneo hilo siku za hivi karibuni kusitisha safari zao mpaka pale watakapopewa taarifa. 

Si mara ya kwanza kwa watu kujaribu kupanda hadi katika kilele cha mnara wa Eiffel. Mwaka 2015, mkimbiaji huru wa Uingereza, James Kingston alipanda bila kamba za usalama wala ruhusa. 

Mnara huo ni mrefu zaidi nchini Ufaransa ukiwa na mita 324 ikiwa ni sawa na jengo la ghorofa 81.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
26 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
26 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
26 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV