Mgomo wa daladala wasitishwa Arusha, Madereva wafunguka mazito

May 26, 2026 12:15 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Wasema LATRA wafanye maboresho haraka kupunguza utitiri wa faini.

Arusha. Hatimaye mgomo wa vyombo vya usafiri ikiwemo daladala umesitishwa rasmi jijini Arusha baada ya Serikali kuahidi kushughulikia baadhi ya changamoto zilizokuwa zikilalamimikiwa.

Kamera ya Nukta Tv leo Mei 26, 2026 imezunguka katika mitaa ya Morombo, Mbauda, Ngusero, Stendi ndogo, Mianzini mpaka Usa River na kujionea shughuli za usafirishaji kupitia daladala zikiendelea kama kawaida.

Mgomo huo uliotikisa kwa siku moja ulitokana na malalamiko ya madereva hao wanaodai kunyanyaswa na maofisa wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini ( LATRA), hususan utozwaji wa faini kubwa zinazofikia kati ya Sh250,000 hadi Sh350,000 kwa magari yanayodaiwa kuzidisha nauli zilizowekwa rasmi na mamlaka hiyo.

Kutokana na hali hiyo, mamia ya wakazi wa jiji la Arusha walilazimika kutumia usafiri wa ziada ikiwemo bajaji, boda boda na guta suala liliohatarisha usalama wao.

Serikali kupitia Mkuu wa Wilaya ya Arusha Joseph Mkude jana ilifanya mazungumzo na wawakilishi wa waendesha daladala na LATRA ambao walikubaliana shughuli za usafiri ziendelee wakati wakishugulikia changamoto hizo zinazolkalamikiwa.

Wakizungumza na Nukta Tv baadhi ya madereva wa daladala wameiomba Serikali kushughulikia kwa haraka changamoto hizo ili wafahamu muafaka wa nauli zinazopaswa kutozwa kulingana na ongezeko la bei ya mafuta.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

/
No matches found for this filter
28 May, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
28 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
28 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA KWENYE MAHAFALI YA MAAFISA NA WAKAGUZI WASAIDIZI WA POLISI

🔴LIVE: RAIS SAMIA KWENYE MAHAFALI YA MAAFISA NA WAKAGUZI WASAIDIZI WA POLISI

Nukta TV

MFAHAMU SUZANA MUSSA, MAMA MZAZI WA HAYATI MAGUFULI

MFAHAMU SUZANA MUSSA, MAMA MZAZI WA HAYATI MAGUFULI

Nukta TV

🔴LIVE: KOMBO AKIWASILISHA BAJETI YA WIZARA YA MAMBO YA NJE BUNGENI 2026/2027

🔴LIVE: KOMBO AKIWASILISHA BAJETI YA WIZARA YA MAMBO YA NJE BUNGENI 2026/2027

Nukta TV