Mgomo wa daladala wasitishwa Arusha, Madereva wafunguka mazito
- Wasema LATRA wafanye maboresho haraka kupunguza utitiri wa faini.
Arusha. Hatimaye mgomo wa vyombo vya usafiri ikiwemo daladala umesitishwa rasmi jijini Arusha baada ya Serikali kuahidi kushughulikia baadhi ya changamoto zilizokuwa zikilalamimikiwa.
Kamera ya Nukta Tv leo Mei 26, 2026 imezunguka katika mitaa ya Morombo, Mbauda, Ngusero, Stendi ndogo, Mianzini mpaka Usa River na kujionea shughuli za usafirishaji kupitia daladala zikiendelea kama kawaida.
Mgomo huo uliotikisa kwa siku moja ulitokana na malalamiko ya madereva hao wanaodai kunyanyaswa na maofisa wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini ( LATRA), hususan utozwaji wa faini kubwa zinazofikia kati ya Sh250,000 hadi Sh350,000 kwa magari yanayodaiwa kuzidisha nauli zilizowekwa rasmi na mamlaka hiyo.
Kutokana na hali hiyo, mamia ya wakazi wa jiji la Arusha walilazimika kutumia usafiri wa ziada ikiwemo bajaji, boda boda na guta suala liliohatarisha usalama wao.
Serikali kupitia Mkuu wa Wilaya ya Arusha Joseph Mkude jana ilifanya mazungumzo na wawakilishi wa waendesha daladala na LATRA ambao walikubaliana shughuli za usafiri ziendelee wakati wakishugulikia changamoto hizo zinazolkalamikiwa.
Wakizungumza na Nukta Tv baadhi ya madereva wa daladala wameiomba Serikali kushughulikia kwa haraka changamoto hizo ili wafahamu muafaka wa nauli zinazopaswa kutozwa kulingana na ongezeko la bei ya mafuta.