Mfumuko wa bei wapaa kwa asilimia 0.1 Agosti 

September 11, 2026 4:08 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Mfumuko wa bei wafikia asilimia 4.3 kwa mwaka ulioishia Agosti 2026 kutoka asilimia 4.2 Julai.
  • Bei wa vyakula washuka hadi asilimia 3.7 kutoka asilimia 4.1.

Dar es Salaam. Kasi ya ongezeko la bei za bidhaa na huduma nchini imeongezeka kwa asilimia 0.1 kwa mwaka ulioishia Agosti 2026  ikichangiwa na kupaa kwa gharama za habari na mawasiliano.

Hii inamaanisha kuwa, kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Agosti, 2026 imeongezeka na kufikia asilimia 4.3 ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia mwezi uliopita. 

Taarifa ya mwenendo wa mfumuko wa bei nchini iliyotolewa Septemba 8, 2026 na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imebainisha kiwango cha mfumuko wa bei Agosti bado kipo ndani ya wastani.

“Kwa ujumla kati ya mwezi Agosti 2025 na Agosti 2026, zikiongezeka kutoka 119.77 hadi 124.93. Katika kipindi hicho kiwango cha Mfumuko wa Bei kiliendelea kuwa katika kiwango cha wastani, kikiwa kati ya asilimia 3.2 na asilimia 4.3,” imesema NBS.

Uchambuzi uliofanywa na Nukta Hababri umebaini kuwa kiwango cha Agosti 2026 ndio cha juu zaidi kuwahi kurekodiwa ndani ya miaka mitatu iliyopita.

Kiwango cha juu zaidi cha mfumuko wa bei kilichorekodiwa ndani ya  kipindi hicho kilikuwa asilimia 4.0 Mei 2023. Katika miezi iliyofuata, kiwango hicho kiliendelea kupanda na kushuka, kikibadilika ndani ya wastani wa kati ya asilimia 3.9 na asilimia 4.2.

Kuanzia Agosti 2023 kurudi nyuma kiwango hicho kilipaa hadi kufikia asilimia 4.9 Oktoba, 2022.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
12 Sep, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
12 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
12 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Jinsi waajiri wanavyokimbilia 'Interns' kukwepa ajira za kudumu

Jinsi waajiri wanavyokimbilia 'Interns' kukwepa ajira za kudumu

Nukta TV

Mtihani darasa la saba kuanza kesho, 1,168,649 wakitarajiwa kuufanya

Mtihani darasa la saba kuanza kesho, 1,168,649 wakitarajiwa kuufanya

Nukta TV

Ajali yaua wanne Dar, watano wafariki mgodi wa dhahabu Gairo

Ajali yaua wanne Dar, watano wafariki mgodi wa dhahabu Gairo

Nukta TV