Meli ya MV Mwanza yaanza majaribio Ziwa Victoria

March 28, 2024 10:57 am · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni jaribio la kwanza kati ya majaribio matatu yanayotakiwa kufanyika.
  • Majaribio hayo yataifanya meli hiyo kukamilika kwa asilimia 96.

Mwanza. Meli mpya ya MV Mwanza iliyokuwa inajengwa katika karakana ya Mwanza Kusini, imeanza kufanyiwa majaribio ya kiufundi kuona iwapo injini na mitambo mingine iliyowekwa ndani ya meli hiyo inafanya kazi kikamilifu.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) Erick Hamis aliyekuwa akizungumza wakati wa majaribio hayo amebainisha kuwa majaribio hayo ya siku tatu yataifanya meli hiyo kukamilika kwa asilimia 96.

Meli hiyo ambayo ni kubwa katika Ukanda wa Afrika Mashariki baada ya kukamilika itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 1,200, tani 400 za mizigo na magari 20 na kati ya hayo matatu ni makubwa.

“Kwa mara ya kwanza toka meli hiyo ilipoanza kujengwa, leo meli hiyo inaanza kufanyiwa majaribio ya kiufundi kuona kama injini zilizowekwa, mitambo yote ya kuongozea meli na vifaa vingine kama vinafanya kazi vizuri,” amesema Hamis.

Muonekano wa meli ya MV Mwanza ikiwa kwenye bandari ya Mwanza Kusini kabla ya kuanza kufanyiwa majaribio. Pichal Mariam John/ Nukta Africa

Mkurugenzi huyo amesema katika majaribio hayo, kuna jopo la wataalamu zaidi ya 60 wakiwemo wakandarasi, wahandisi, wataalamu wa MSCL na wasambazaji wa mashine mbalimbali kutoka Marekani na China ambao wataangalia mashine zao zinavyofanya kazi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya MSCL, John Mbungo amesema ni wakati sasa kwa Wizara ya Viwanda kutumia fursa hiyo kwa kuwa na mikakati ya kuanza uzalishaji mitambo mingine.

“Tayari tumeshuhudia meli hii ikiundwa hapa hapa nchini, hivyo wataalamu wapo na tunaweza hata kuunda magari hapa hapa nchini,” amesema Mbungo

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV