Mchuano mkali watoa huduma za ving’amuzi Tanzania

June 3, 2021 8:40 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Startimes yaendelea kumiliki soko kwa zaidi ya asilimia 60.
  • Hadi kufikia mwaka 2020, ving’amuzi vilivyokuwa vinafanya kazi vilikuwa milioni 2.8.

Dar es Salaam. Uchambuzi wa takwimu za robo ya kwanza ya mwaka 2021 za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) umebaini kuwa idadi ya ving’amuzi vinavyonunuliwa inaongezeka kila mwaka nchini Tanzania lakini changamoto ipo kwenye matumizi yake.

Vipo ambavyo vinanunuliwa na watu lakini havitumiki kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo baadhi ya kushindwa kulipia malipo ya kila mwezi ili kuendelea chaneli kwenye televisheni zao.

Kwa mujibu wa TCRA, hadi kufikia mwaka 2020, ving’amuzi vinavyofanya kazi ambavyo vinatumiwa na Watanzania vimefikia milioni 2.8 ambapo zaidi ya nusu wanatumia king’amuzi cha Startimes. 

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW