Mapato ya Apple, Amazon yapaa
- Mapato ya Apple yapanda kwa asilimia 2 robo ya tatu ya 2022.
- Amazon mapato yake yaongezeka kwa asilimia 7.
- Ni kutokana kuongezeka kwa bidhaa za kampuni hiyo.
Kampuni ya teknolojia na vifaa vifaa vya kielektroniki ikiwemo simu ya Apple imesema mauzo ya bidhaa na huduma zake yameongezeka kwa asilimia mbili hadi kufikia Dola za Marekani bilioni 83 sawa na Sh 193.5 trilioni katika robo ya tatu ya mwaka 2022.
Afisa Mkuu wa Fedha wa kampuni hiyo inayotengeneza simu za iPhone, Luca Maestri katika taarifa yake ya Julai 28, 2022 amesema wamepta mafanikio hayo katika kipindi ambacho nchi nyingi duniani zinakumbana na changamoto za kushuka kwa uchumi na athari ya mgogoro wa vita ya Urusi na Ukraine.
Simu na huduma za Iphone zimeendelea kuwa na hitaji kubwa kwa wateja huku huduma za malipo (Apple Pay) na mauzo ya muziki mtandaoni (iTunes) yakiongezeka kwa asilimia 12 ikilinganishwa na ripoti ya awali.
Pia kampuni ya Amazon inayoshughulika na biashara za mtandaoni, uchukuzi wa kidijitali imeripoti ongezeko la mapato kwa asilimia 7 kufikia Dola za Marekani bilioni 121.2 sawa na Sh282.1 trilioni ingawa mauzo ya mtandaoni yamepungua kwa asilimia 4 kwa mwaka.
Amazon imeendelea kupata faida kupitia ya asilimia 33 ya mauzo ya huduma za mtandao (AWS), komputa anga (cloud computing division) na akili bandia (Artificial Intelligence)
“Licha kuendelea kupanda kwa gharama za mafuta, nishati na gharama za usafirishaji, tunapiga hatua zaidi kwenye gharama zinazoweza kudhibitika hasa katika kuboresha mtandao wa utimilifu” alisema Andy Jassy afisa mtendaji wa Amazon.
Latest
