Mapambano dhidi ya Ukimwi yashika kasi Tanzania
- Wizara ya Afya imekusudia kubaini waishio na VVU bila kujitambua.
- Kupunguza idadi ya watoto wanaozaliwa na Virusi Vya Ukimwi kuwa miongoni mwa mapambano.
Dar es Salaam. Wizara ya Afya imesema inakusudia kupunguza idadi ya watoto wachanga wanaozaliwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) kutoka 6000 wanaozaliwa kila mwaka kwa kuhakikisha inamfikia kila mwanamke mwenye ujauzito.
Hayo yamesemwa Januari 20, 2022 na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu wakati alipokuwa akizindua mpango mkakati wa miaka mitano wa tafiti na mafunzo katika masuala ya afya ya jamii na lishe.
“Nchini Tanzania inakadiriwa watu milioni 1.7 wanaoishi na Virusi vya Ukimwi lakini wanaotambua hali zao za afya ni milioni 1.5 pekee, hii ni changamoto kwetu lazima tuwatafute hawa 200,000 kwani ndiyo wanaochangia maambukizi mapya bila kujua,” amesema Waziri wa Afya
Amesema suala la mtoto kuzaliwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi halikubaliki.

Latest