Mikoa inayoongoza maambukizi ya VVU Tanzania

August 3, 2024 9:37 am · Esau Ng'umbi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Licha ya jitihada za kupunguza maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi (VVU), bado kuna baadhi ya mikoa nchini ina kiwango kikubwa cha maambuzi ya VVU, mara 2 zaidi ya wastani wa kitaifa wa 4.4% kwa mujibu wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi 2022-23 wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu ( NBS).

Maambukizi ya VVU Tanzania yamepungua ndani ya miaka 19 kutoka 7% mwaka 2003/04 hadi 4.4% mwaka 2022-23. 

Hali ya maambukizi ya VVU kwa watu wenye miaka 15 au zaidi mwaka 2022/23 kitaifa ni asilimia 4.4% wanawake wakiwa na asilimia 5.6 na wanaume asilimia 3.0. Hii ina maana kuwa kitaifa watu 44 kati ya 1,000 wenye miaka 15 au zaidi wana maambukizi ya maradhi hayo. Kwa jinsia, hii ina maana kuwa wanawake 56 kati ya 1,000 wana VVU wenye umri huo ikilinganisha na wanaume 30 kwa kila 1,000.

Vijana ni miongoni mwa waathirika wakubwa wa maradhi hayo ammbapo miongoni mwa mipango ya Serikali ya Tanzania kwa sasa ni kupunguza maambukizi mapya hususan kwa vijana balehe pamoja na kupunguza maambukizi mapya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Unafikiri ni kwa nini mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya, Songwe na Kagera ina viwango vikubwa vya maambukizi ya VVU Tanzania?

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
WAMESANUKA, mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa za kulevya yafichuliwa

WAMESANUKA, mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa za kulevya yafichuliwa

Nukta TV

CCM yatoa ratiba maombi ya kumrithi Lukuvi, Israel, Lebanon wakisitisha mapigano

CCM yatoa ratiba maombi ya kumrithi Lukuvi, Israel, Lebanon wakisitisha mapigano

Nukta TV

Ridhiwani: Serikali inalenga kuacha tabasamu kwa watumishi wa Umma

Ridhiwani: Serikali inalenga kuacha tabasamu kwa watumishi wa Umma

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.