Mikoa inayoongoza maambukizi ya VVU Tanzania

August 3, 2024 9:37 am · Esau Ng'umbi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Licha ya jitihada za kupunguza maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi (VVU), bado kuna baadhi ya mikoa nchini ina kiwango kikubwa cha maambuzi ya VVU, mara 2 zaidi ya wastani wa kitaifa wa 4.4% kwa mujibu wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi 2022-23 wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu ( NBS).

Maambukizi ya VVU Tanzania yamepungua ndani ya miaka 19 kutoka 7% mwaka 2003/04 hadi 4.4% mwaka 2022-23. 

Hali ya maambukizi ya VVU kwa watu wenye miaka 15 au zaidi mwaka 2022/23 kitaifa ni asilimia 4.4% wanawake wakiwa na asilimia 5.6 na wanaume asilimia 3.0. Hii ina maana kuwa kitaifa watu 44 kati ya 1,000 wenye miaka 15 au zaidi wana maambukizi ya maradhi hayo. Kwa jinsia, hii ina maana kuwa wanawake 56 kati ya 1,000 wana VVU wenye umri huo ikilinganisha na wanaume 30 kwa kila 1,000.

Vijana ni miongoni mwa waathirika wakubwa wa maradhi hayo ammbapo miongoni mwa mipango ya Serikali ya Tanzania kwa sasa ni kupunguza maambukizi mapya hususan kwa vijana balehe pamoja na kupunguza maambukizi mapya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Unafikiri ni kwa nini mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya, Songwe na Kagera ina viwango vikubwa vya maambukizi ya VVU Tanzania?

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV