Makala kuenzi utendaji kazi wa Makonda, Kenani Arusha

August 29, 2025 5:58 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Aahidi kufanya ziara kila kata kutatua changamoto za wananchi

Arusha. Mkuu wa Mkoa wa mpya wa Arusha Amosi Makala, ameahidi kusikiliza kero za wananchi katika kila kata kama ilivyokuwa ikifanyika na watangulizi wake Paul Makonda pamoja na Kenani Kihongosi.

Agosti 23 mwaka huu Rais Samia Suluhu Hassan alimteua Makala kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha akimrithi Kenani Kihongosi aliyeongoza jiji hilo kwa miezi miwili.

Makala ametoa ahadi hiyo alipokuwa akipokelewa rasmi katika ofisi za mkuu wa mkoa jijini humo leo Agosti 29, 2025 akisisitiza kuwa atawatumikia wananchi kwa kuwafuata katika kata na wilaya zao na kutatua kero zilizopo.

“Nitawafuata mlipo wale wanaodhani wakija kwa Mkuu wa Mkoa mara kwa mara watanikuta ofisini siyo hiyo….mimi napenda kufanya kazi na wananchi tunataka kuwasikiliza wananchi tunataka kutatua kero za wananchi,” amesema Makala.

Aina hiyo ya utendaji kazi ya kusikiliza kero za wananchi iliwahi kufanywa na aliyekuwa mkuu wa mkoa huo, Paul Makonda ambaye kwa sasa ni mgombea ubunge wa jimbo la Arusha kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na kuendelezwa na Kenani Kihongosi.

Makala amebainisha kuwa ziara ayake ya kwanza itakuwa katika Wilaya ya Ngorongoro ambayo kwa mujibu wake viongozi wengi walikuwa hawafiki mara kwa mara.

Aidha, Makala amewataka wananchi wa mkoa huo kudumisha amani ili kuendelea kuvutia utalii ambao ni kitovu cha uchumi wa jiji hilo.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.