Makala kuenzi utendaji kazi wa Makonda, Kenani Arusha
- Aahidi kufanya ziara kila kata kutatua changamoto za wananchi
Arusha. Mkuu wa Mkoa wa mpya wa Arusha Amosi Makala, ameahidi kusikiliza kero za wananchi katika kila kata kama ilivyokuwa ikifanyika na watangulizi wake Paul Makonda pamoja na Kenani Kihongosi.
Agosti 23 mwaka huu Rais Samia Suluhu Hassan alimteua Makala kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha akimrithi Kenani Kihongosi aliyeongoza jiji hilo kwa miezi miwili.
Makala ametoa ahadi hiyo alipokuwa akipokelewa rasmi katika ofisi za mkuu wa mkoa jijini humo leo Agosti 29, 2025 akisisitiza kuwa atawatumikia wananchi kwa kuwafuata katika kata na wilaya zao na kutatua kero zilizopo.
โNitawafuata mlipo wale wanaodhani wakija kwa Mkuu wa Mkoa mara kwa mara watanikuta ofisini siyo hiyoโฆ.mimi napenda kufanya kazi na wananchi tunataka kuwasikiliza wananchi tunataka kutatua kero za wananchi,โ amesema Makala.

Aina hiyo ya utendaji kazi ya kusikiliza kero za wananchi iliwahi kufanywa na aliyekuwa mkuu wa mkoa huo, Paul Makonda ambaye kwa sasa ni mgombea ubunge wa jimbo la Arusha kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na kuendelezwa na Kenani Kihongosi.
Makala amebainisha kuwa ziara ayake ya kwanza itakuwa katika Wilaya ya Ngorongoro ambayo kwa mujibu wake viongozi wengi walikuwa hawafiki mara kwa mara.
Aidha, Makala amewataka wananchi wa mkoa huo kudumisha amani ili kuendelea kuvutia utalii ambao ni kitovu cha uchumi wa jiji hilo.
Latest
