Majina waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano 2020 bayana

June 17, 2020 12:05 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Wanafunzi 121,251 wamechaguliwa kujiunga na ngazi hizo za elimu wakiwemo wasichana 53,829.
  •  Katika majina hayo mapya, aliyekuwa mwanafunzi bora kitaifa katika mtihani wa kidato cha nne, Joan Ritte amechaguliwa kujiunga na shule ya vipaji maalum ya Kilakala iliyopo mkoani Morogoro.

Dar es Salaam. Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imetoa orodha ya majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano, vyuo vya ufundi na ualimu kwa mwaka 2020 ikiwa ni dakika chache baada ya Serikali kutangaza utaratibu wa kurejea shuleni kwa wanafunzi waliokuwa wamefunga shule kutokana na ugonjwa wa virusi vya corona. 

Waziri wa Ofisi ya Rais-Tamisemi Suleiman Jafo amewaambia wanahabari Jumatano (Juni 17, 2020) kuwa wanafunzi 121,251 wamechaguliwa kujiunga na ngazi hizo za elimu wakiwemo wasichana 53,829. 

Wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na shule za bweni wanatakiwa kuripoti shuleni Julai 18, 2020 ili kuanza masomo Julai 20, Jafo amesema. 

Wanafunzi waliomaliza kidato cha nne mwaka jana walikuwa wakisubiri kwa hamu taarifa hizo ambazo ni muhimu katika safari yao ya kupata elimu ya juu nchini. 


Zinazohusiana:


Katika majina hayo mapya, aliyekuwa mwanafunzi bora kitaifa katika mtihani wa kidato cha nne, Joan Ritte amechaguliwa kujiunga na shule ya vipaji maalum ya Kilakala iliyopo mkoani Morogoro.

Ritte amechaguliwa kusoma mchepuo wa PCM ukihusisha Fizikia, Kemia na Hisabati. 

Mbali na kuwachagua wanafunzi kwenda kidato cha tano, Tamisemi imewachagua wanafunzi kwenda kusoma astashahada mbalimbali katika vyuo vya umma ikiwemo stashahada ya awali ya ualimu.

Majina hayo yametangazwa dakika chache baada ya wizara ya elimu, sayansi na teknolojia kutangaza utaratibu wa kurejea kwa masomo kwa wanafunzi wote waliokuwa wamefunga shule kutokana na ugonjwa wa virusi vya corona ikiwemo shule za msingi na awali.

Kufahamu mwanafunzi amechaguliwa kwenda shule au chuo gani bonyeza hapa

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV