Majaliwa atoa tahadhari msimu mpya ununuzi wa korosho 2019

October 3, 2019 6:03 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Amewaagiza wakuu wa mikoa inayolima zao hilo wasiruhusu kuingizwa kwa mfumo mpya wa ununuzi ambao haujaeleweka kwa wadau na wanunuzi.
  •  Msimu wa korosho kwa mwaka huu unatarajiwa kutangazwa hivi karibuni.
  • Watakaotumia kangomba kununua korosho, moto utawawakia.  

Dar es Salaam. Wakati msimu wa korosho kwa mwaka 2019 ukitarajia kutangazwa hivi karibuni, Serikali amewaagiza wakuu wa mikoa inayolima zao hilo wasiruhusu kuingizwa kwa mfumo mpya wa ununuzi ambao haujaeleweka kwa wadau na wanunuzi.  

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliyekuwa akizungumza jana (Oktoba 2, 2019) mkoani Mtwara amesema msimu wa korosho kwa mwaka huu unatarajiwa kutangazwa hivi karibuni, hivyo ni vema wakuu wa mikoa inayolima korosho wakajiandaa vizuri ili kuepusha migogoro isiyokuwa ya lazima.

“Mabadiliko  ya mifumo yalitolewa na baadhi ya viongozi ambao siyo waaminifu, Serikali iko macho itawachukulia hatua viongozi wa vyama vya ushirika wasiokuwa waaminifu. Tunataka mfumo wenye manufaa ndiyo utumike,” amesema Majaliwa.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Serikali imewataka wafanyabiashara kutojihusisha na ununuzi wa korosho kwa njia ya zisizo halali ikiwemo kangomba.

”Kangomba imepigwa marufuku, watakaojihusisha moto utawawakia huko huko . Tunataka wakulima wenyewe ndio wanufaike,” amesema Majaliwa jana alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini iliyopo Mtwara.


Zinazohusiana:


Pia, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wakulima wa korosho kuendelea kujiimarisha na wahakikishe wanajiwekea akiba kwa ajili ya ununuzi wa pembejeo. 

Awali, Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha kubangua korosho cha Yalin kilichopo katika eneo la Msijute mkoani Mtwara na kukagua kazi ya ubanguaji pamoja na kuzungumza na watumishi wa kiwanda hicho ambao waliishukuru Serikali kwa kuhamasisha ujenzi wa viwanda.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV