Majaliwa ataja manufaa ya mpango kabambe wa uvuvi

September 20, 2022 2:06 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Utasaidia kukuza sekta hiyo na kuongeza mchango wake katika pato la Taifa hadi kufikia asilimia 10 kwa mwaka kutoka asilimia 1.8 ya sasa.  

Dar es Salaam. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema utekelezaji wa Mpango Kabambe wa Sekta ya Uvuvi utasaidia kukuza sekta hiyo na kuongeza mchango wake katika pato la Taifa hadi kufikia asilimia 10 kwa mwaka kutoka asilimia 1.8 ya sasa.  

Majaliwa amesema kuwa mpango huo ambao utakaotekelezwa kwa kipindi cha miaka 15 kuanzia 2021/22 hadi 2036/37 una umuhimu mkubwa  katika ukuaji wa sekta ya uvuvi pamoja na uchumi wa buluu.  

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwahakikishia wadau wote wa sekta ya uvuvi kuwa Serikali ina nia ya dhati ya kuhakikisha kila mmoja ananufaika na sekta hiyo. 

Amesema hayo leo Septemba 20, 2022 wakati wa uzinduzi wa Mpango Kabambe wa Sekta ya Uvuvi, katika ukumbi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam jijini Dar es Salaam.  

“Tutaendelea kupokea mapendekezo yenu ili tuweze kuboresha sekta hii, ubunifu wenu ni muhimu, wote tunataka tuzungumze lugha moja,” amesema Majaliwa.

                     

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW