Kesi ya mwanahabari Erick Kabendera yapigwa kalenda

August 19, 2019 8:23 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu ya Mkazi Kisutu leo (Agosti 19, 2019) lakini kesi yake haikusikilizwa. 
  • Amerudishwa  rumande hadi Agosti 30, 2019 baada ya Hakimu anayesikiliza kesi yake kupata udhuru.
  • Upande wa mashtaka bado haujakamilisha upelelezi wa kesi hiyo.  

Dar es Salaam. Mwandishi habari za uchunguzi, Erick Kabendera anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi na kutakatisha pesa amerudishwa  kwa siku 12 baada ya hakimu anayesikiliza kesi yake kupata udhuru. 

Kabendera alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu ya Mkaazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo (Agosti 19, 2019) lakini kesi yake haikusikilizwa baada ya mahakama hiyo kueleza kuwa Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Rwezile amepata udhuru. 

Hata hivyo, upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na Wakili Wankyo Simon nao umesema haujakamilisha upelelezi na kuomba kesi hiyo ipangiwe siku nyingine wakati wakikamilisha uchunguzi. 

Kutokana na sababu hizo mbili, Kabendera amerudishwa rumande hadi Agosti 30, 2019  kabla ya kupandishwa tena kizimbani.


Soma zaidi: 


Akizungumza nje ya Mahakama, Wakili wa Kabendera, Jebra Kambole amesema hawana tatizo na hakimu kupata udhuru lakini wanauomba upande wa jamhuri kukamilisha upelelezi kwa wakati ili kesi iendelee kwa sababu mashtaka yanayomkabili mteja wake hayana dhamana. 

Mashtaka yanayomkabili mwanahabari huyo ni kuongoza kundi la uhalifu kwa lengo la kupata faida au manufaa mengine, kutokulipa kodi kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ya zaidi ya Sh173.24 milioni na utakatishaji wa fedha kiasi cha  zaidi ya Sh173.24 milioni.

Kabendera, ambaye anaandikia  vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi alichukuliwa kwa nguvu nyumbani kwake Mbweni Jijini Dar es Salaam Julai 29, 2019 na watu waliojitambulisha kuwa ni polisi na tangu wakati huo amekuwa akishikiliwa na polisi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
17 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Msemaji Geita: Vijana msikurupuke kuja Katoro

Msemaji Geita: Vijana msikurupuke kuja Katoro

Nukta TV

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV