Jinsi ya kupika wali wa manjano 

July 30, 2022 10:55 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Mbali na rangi yake wali huu una faida nyingi mwilini.
  • Unachohitaji ni mchele, manjano na kitunguu swaumu.
  • Mahitaji mengine ni kitunguu maji, chumvi na mafuta.

Manjano ni kiungo cha asili ambacho kinatumika kwenye mapishi ya aina mbalimbali na urembo wa ngozi na nywele.

Uwepo wa kiambata cha calcium hukipa kiungo hicho rangi ya njano ambayo huenda ndiyo chanzo cha jina la kiungo hicho kufanana na rangi yake.

Mbali na faida kwenye nywele na ngozi jarida la habari za kitabibu la Medical News today, linasema kiungo hicho kina viambata vya  kuzuia uvimbe, kuzuia magonjwa ya moyo na kansa pamoja na kuongeza kinga ya mwili.

Basi nikukaribishe jikoni, nikupe usukani wa kupika  pishi hili ambalo mbali na kukupatia shibe na ladha ya kipekee, litaboresha afya yako na kukusaidia kupambana na magonjwa.

Utakachokihitaji ni mchele, manjano vijiko viwili, kitunguu swaumu, kitunguu maji na chumvi. Pishi hili unaweza kula kwa mboga yoyote iwe nyama, kachumbari au mboga za majani.

Maandalizi

Chambua mchele, uoshe na uuchuje maji, kisha menya kitunguu swaumu na utwange mpaka kilainike. Osha na ukatekate kitunguu maji kwa saizi ya urefu.

Washa jiko na uchemshe maji kwa ajili ya kupikia wali, yakichemka yaipue na uyahifadhi. Katika sufuria nyingine weka mafuta kiasi kaanga kitunguu swaumu pamoja na kitunguu maji mpaka viwe na rangi ya kahawia.

Ongeza manjano, koroga ili yachanganyike vizuri kisha ingeza chumvi, mchele na maji uliyoyachemsha kiasi cha kuweza kuivisha wali wako.

Funika na usubiri wali uive, hapa unaweza kuongeza iriki au mdalasini kama unapendelea.

Wali ukiiva, rangi itabadilika na kuwa ya njano na hapo wali wa manjano utakuwa kwa tayari kwa kuliwa. 

Wali huu unaweza kuliwa na mboga yoyote, ikiwemo nyama , samaki na mboga za majani.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV