JKT yatangaza nafasi za mafunzo ya kujitolea kwa vijana 2026

January 20, 2026 5:26 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Usaili utaanza rasmi Januari 26, 2026 katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani na vijana watakaoteuliwa wanatakiwa kuripoti katika kambi husika kuanzia Februari 27 hadi 4 Machi 2026.

Dar es Salaam. Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limetangaza nafasi za kujiunga na mafunzo ya kujitolea kwa mwaka 2026 kwa vijana wote wa Tanzania Bara na Visiwani, hatua inayolenga kuwajengea vijana uzalendou, ukakamavu na stadi za maisha.

Taarifa ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Rajabu Mabele iliyotolewa leo Januari 20, 2026 inabainisha kuwa vijana wanaohitajika ni wenye taaluma mbalimbali.

“Vijana wenye Vipaji vya Michezo mbalimbali, wanashauriwa kujitokeza kwa wingi kupitia Mikoa yao,” imeeleza taarifa ya Jenerali Mabele.

Mabele amesema utaratibu wa kujiungana mafunzo unaratibiwa kupitia Ofisi za Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambako waombaji wanaishi huku sifa kuu za waombaji zikizorodhesha katika tovuti rasmi ya jeshi hilo.

Pamoja na jeshi hilo kuwaita wenye vipaji pia liimewahimiza vijana wenye Stashahada au Shahada katika taaluma mbalimbali ikiwemo teknolojia ya habari (Tehama), sayansi ya kompyuta, uhandisi wa kompyuta, mifumo ya taarifa za biashara, usalama wa mtandao na uchunguzi wa kidijitali pamoja na mitandao ya kompyuta na uhandisi wa usalama wa taarifa kujitokeza kwa wingi. 

Usaili wa kuwapata vijana watakaojiunga na mafunzo ya JKT kwa kujitolea utaanza rasmi Januari 26, 2026 katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani na vijana watakaoteuliwa wanatakiwa kuripoti katika kambi husika kuanzia Februari 27 hadi 4 Machi 2026.

Mafunzo hayo hayatoi ajira

Hata hivyo, JKT limeweka wazi kuwa mafunzo hayo hayatoi ajira wala halihusiki kuwatafutia ajira wahitimu wake katika taasisi, vyombo vya ulinzi na usalama au mashirika ya Serikali na yasiyo ya kiserikali. 

Badala yake, JKT hutoa mafunzo yanayolenga kuwawezesha vijana kujiajiri wenyewe baada ya kumaliza mkataba wao.

Kwa mujibu wa JKT vifaa wanavyotakiwa kwenda navyo vijana hao wakati wa kuripoti vimeanishwa katika tovuti rasmi ya JKT ambayo ni www.jkt.mil.tz

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV