INEC yatangaza ratiba mpya uchaguzi udiwani Kata za Mindu, Mzinga, Kirua

October 24, 2025 3:05 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Uchaguzi katika kata hizo kufanyika Jumatano Januari 5, 2026.
  •  Uteuzi mpya hautahusisha mgombea mwingine yeyote aliyeteuliwa kihalali katika uteuzi uliofanyika awali.

Dodoma.Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza mabadiliko ya ratiba ya uchaguzi wa madiwani katika Kata ya Mindu (Jimbo la Morogoro Mjini), Kata ya Mzinga (Jimbo la Kivule) na Kata ya Kirua Vunjo Magharibi (Jimbo la Vunjo).

Uamuzi huo umetokana na vifo vya wagombea watatu waliokuwa wakiwania nafasi za udiwani katika kata hizo.

Taarifa iliyotolewa leo Oktoba 24, 2025 na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Ramadhani Kailima, imeeleza kuwa kwa mujibu vifungu vya sheria ya uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani ya mwaka 2024, uchaguzi katika jimbo hilo ulisitishwa rasmi Oktoba 21, 2025.

Taarifa hiyo, imebainisha kuwa fomu za uteuzi katika kata hizo zitatolewa Oktoba 28, 2025 hadi Novemba 3,2025 kwa wagombea udiwani wa Chama cha mapinduzi (CCM), Chama cha The Civic United Front (CUF), na Chama cha ACT Wazalendo.

Baada ya uchukuaji wa fomu hizo, siku hiyo hiyo ya Novemba 3 kutafanyika uteuzi wa mgombea kupitia vyama hivyo.

Kulingana na taarifa hiyo, kampeni za uchaguzi wa madiwani katika kata hizo zitafanyika kuanzia Novemba 4, 2025 hadi Januari 4, 2026 na uchaguzi kufanyika siku ya Jumatano Januari 5, 2026.

Aidha, tume imefafanua kuwa uteuzi mpya hautahusisha mgombea mwingine yeyote aliyeteuliwa kihalali katika uteuzi uliofanyika awali isipokuwa kama atatoa taarifa ya kujitoa.

Wagombea hao waliofariki ni pamoja na Hamisi Mohamedi Msasa (ACT-Wazalendo) aliyefariki Oktoba 17,2025, Rashid Abdallah Nandonde (CUF) Oktoba 19, 2025 na John Boniface Kessy (CCM) aliyefariki Oktoba 21, 2025.

Aidha, tume imevikumbusha vyama vya siasa, wagombea na wadau wa uchaguzi kuendelea kuzingatia katiba ya Tanzania, sheria za uchaguzi, kanuni, maadili, taratibu, miongozo na maelekezo yatakayotolewa na tume katika kufanikisha ratiba ya uchaguzi husika.

Taarifa hii ya INEC inakuja ikiwa zimebaki siku tano pekee zoezi la upigaji kura kuchukua nafasi yake ifikapo Oktoba 29, 2025.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV