INEC yamuondoa tena Mpina kwenye kinyang’anyiro cha Urais Tanzania
- Ni baada ya kushinda kesi ya dhidi ya INEC siku nne zilizopita
Arusha. Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imemuondoa tena Luhaga Mpina kwenye kinyanganyiro cha urais wa Tanzania kupitia chama cha ACT Wazalendo.
Uamuzi huo wa INEC unakuja ikiwa ni siku nne tangu Mpina ashinde kesi dhidi ya tume hiyo kuhusu shauri la maombi ya Kikatiba akipinga kuenguliwa katika mchakato wa uteuzi wa wagombea wa nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025 na siku mbili tangu INEC imteue kuwa mgombea Urais.
Taarifa ya Mkurugenzi wa Uchaguzi Ramadhani Kailima, iliyotolewa leo Septemba 15, 2025 inabainisha kuwa uamuzi huo umetokana na pingamizi lililowasilishwa na Hamza Saidi Johari, Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
“Hivyo, jina la Ndugu Luhaga Joelson Mpina, mgombea wa kiti cha Raiskupitia Chama cha ACT-Wazalendo limeondolewa kwenye orodha ya wagombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025,” imesema Taarifa ya Kailima.
Aidha, INEC imetupilia mbali pingamizi la Mpina dhidi ya Samia Suluhu mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kesi nyingine mbili.
Mapingamizi hayo ni pamoja na lililowekwa na Almas Hassan Kisabya mgombea wa kiti cha Rais kupitia Chama cha NRA dhidi ya Ndugu Luhaga Joelson Mpina mgombea wa Kiti cha Rais kupitia Chama cha ACT Wazalendo
Pingamizi lingine ni lile lililowekwa na Kunje Ngomale Mwiru mgombea kiti cha Rais kupitia chama cha AAFP dhidi ya Ndugu Luhaga Joelson Mpina mgombea wa Kiti cha Rais kupitia Chama cha ACT Wazalendo.
Latest