IMF yasema uchumi wa dunia hautakua kama ilivyotabiriwa Januari 2023

April 12, 2023 7:02 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link

Kwa wapenzi wa samaki aina ya kambale waliokaushwa vizuri, hiyo nayo ni fursa ya kuinua maisha ya akina mama wa soko la Soni la Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga. Picha| K15 Photos.


  • Makadirio ya ukuaji wa uchumi yatakuwa chini kwa asilimia 0.1.
  • Hiyo ni kutokana na kuongezeka kwa mfumuko wa bei za bidhaa na athari za Uviko-19.
  • Uchumi wa dunia kukua kwa asilimi 3 mwaka 2024. 

Dar es Salaam. Shirika la Fedha Duniani (IMF) limesema makadirio ya ukuaji wa uchumi wa dunia kwa mwaka 2023 yatakuwa chini kwa asilimia 0.1 tofauti ilivyotabiriwa mwanzoni mwa mwaka huu.

Hata hivyo, IMF imesema uchumi wa dunia utaimarisha zaidi mwaka ujao wa 2024.

Shirika hilo katika taarifa yake iliyotolewa Aprili 11 mwaka huu limesema ukuaji wa pato la dunia unatarajia kushuka kutoka asilimia 3.4 mwaka jana hadi asilimia 2.8 mwaka wa 2023, kabla ya kupanda hadi asilimia 3 mwaka 2024.

Nchi zenye uchumi mkubwa zinatarajia kushuhudia kushuka kwa ukuaji kutoka asilimia 2.7 mwaka wa 2022 hadi asilimia 1.3 mwaka wa 2023. 

“Mfumuko wa bei wa kimataifa unatarajiwa kushuka kutoka asilimia 8.7 mwaka 2022 hadi asilimia 7 mwaka huu wa 2023 kwa kushuka bei ya bidhaa lakini mfumuko wa bei unaonekana kuwa mbaya zaidi. Muhimu zaidi, matatizo ya hivi karibuni ya kifedha yanabakia yanadhibitiwa,” amesema Pierre-Olivier Gourinchas, Mchumi Mkuu wa IMF

Uchumi wa dunia bado unaendelea kuimarika kutoka kwenye athari za Uviko-19 za miaka mitatu iliyopita ambazo ziliathiri zaidi sekta za uzalishaji na utalii ambazo huchangia kwa sehemu kubwa mapato na ajira katika nchi mbalimbali. 

Kutokuwa na uhakika kunafunika mtazamo wa muda mfupi na wa kati kwa kadri uchumi wa dunia unavyobadilika kulingana na majanga ya mwaka 2020 hadi 2022 na mtikisiko wa sekta ya fedha wa hivi karibuni. 

Wasiwasi wa kushuka kwa uchumi umeongezeka, huku wasiwasi juu ya mfumuko wa bei uliokithiri ukiendelea katika maeneo mbalimbali duniani.

Licha ya mfumuko wa bei kuwa juu katika nchi mbalimbali kwa Tanzania ni tofauti kwa sababu ni himilivu. Mathalan, mfumuko wa bei za bidhaa na huduma muhimu kwa mwaka unaoishia Machi 2023 ulikuwa asilimia 4.7 ukishuka kutoka asilimia 4.8 wa mwaka unaoishia Februari 2023.

Mchumi huyo amesema huenda kukawa na haja ya kubana zaidi fedha ikiwa mfumuko wa bei utaendelea kusalia kuliko inavyotarajiwa. 

Hatari hizi na zaidi zinaweza kutokea wakati watunga sera wanakabiliwa na nafasi finyu zaidi ya sera ili kukabiliana na misukosuko hasi, hasa katika nchi zenye kipato cha chini. 


Zinazohusiana:


Nini kifanyike?

“Kwanza, ilimradi tu matatizo ya kifedha sio ya kimfumo kama ilivyo sasa, vita dhidi ya mfumuko wa bei inapaswa kubaki kuwa kipaumbele kwa benki kuu. Pili, ili kulinda utulivu wa kifedha, benki kuu zinapaswa kutumia zana tofauti na kuwasilisha malengo yao kwa uwazi ili kuepusha hali tete zisizohitajika. 

Sera za kifedha zinapaswa kusalia kulenga uthabiti wa kifedha na kutazama hatari zozote katika benki, zisizo za benki na sekta za mali isiyohamishika,” ameshauri Gourinchas huku akizitaka Serikali kupunguza shinikizo la mfumuko wa bei, kurejesha uhimilivu wa deni, na kujenga upya ulinzi wa kifedha. 

Pia soko linaloibukia na nchi zinazoendelea kiuchumi zinapaswa kutumia mfumo jumuishi wa sera, kuchanganya afua za fedha za kigeni zinazolengwa kwa muda na hatua za mtiririko wa mtaji pale inapobidi. 

Mkurugenzi wa Idara ya Fedha na Masoko ya Mitaji wa IMF, Tobias Adrian amesema bado kuna kazi kubwa ya kufanya kwa sababu bado sekta ya benki haijaimarika, hali ngumu ya maisha na udhaifu wa sekta ya fedha bado unaongezeka.

“Majibu ya haraka na yenye nguvu ya sera yalipunguza wasiwasi wa soko, lakini hisia bado ni tete. Matatizo bado yanaonekana katika taasisi zingine, wawekezaji wanapotathmini upya afya ya mfumo wa kifedha.

Kuibuka kwa msongo katika masoko ya fedha pia kunatatiza kazi ya benki kuu zinapojaribu kudumisha njia ya kufikia viwango vya juu vya riba katika kukabiliana na mfumuko wa bei wa juu,” amesisitiza Adrian. 

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Nukta TV

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Nukta TV

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Nukta TV