Huduma za Google zapata hitilafu

December 14, 2020 12:13 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Baadhi ya watumiaji wake wanalalamika kutopata huduma hizo mtandaoni.
  • Mpaka sasa haijulikani ni sababu gani ambazo zimesababisha hali hiyo. 

Dar es Salaam. Baadhi ya huduma za kampuni ya teknolojia ya Google ikiwemo baruapepe ya Gmail hazipatikani mtandaoni, jambo ambalo limeibua usumbufu kwa watumiaji wa huduma hizo.

Huduma nyinginge ambazo baadhi ya watu wanalalamika kutozipata kuanzia mchana wa leo Desemba 14, 2020 ni mtandao wa YouTube, sehemu ya kuhifadhia nyaraka mtandaoni ya Google Drive na Google doc inayotumika kuandikia nyaraka mbalimbali.

Kwa kila anayetaka kufungua huduma hizo anakutana na ujumbe unaosema ” Samahani, akaunti yako haipatikani. Samahani kwa usumbufu uliotokea na jaribu tena baadaye.”

Mpaka sasa haijulikani ni changamoto gani imetokea kwa huduma hizo kutopatikana.

Pia watumiaji katika mataifa mengine wamelalamika kwa kukosa huduma hizo.


Soma zaidi:


Google imewaelekeza watumiaji wa huduma zake kutembelea kituo cha msaada cha kampuni hiyo yenye makao makuu nchini Marekani kwa ajili ya kupata taarifa zaidi.

Mtandao wa YouTube ni moja ya huduma maarufu ya Google inayowapatia fursa watumiaji wa mtandao kutazama na kusikiliza muziki na kupata habari za televisheni mtandao.

Pia, Google imekua ni kiungo muhimu kwa watu wanaofanyia kazi au biashara mtandaoni kwa sababu ni njia ya rahisi ya kuwasiliana na kutunza nyaraka.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV