Huduma za Google zapata hitilafu

December 14, 2020 12:13 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Baadhi ya watumiaji wake wanalalamika kutopata huduma hizo mtandaoni.
  • Mpaka sasa haijulikani ni sababu gani ambazo zimesababisha hali hiyo. 

Dar es Salaam. Baadhi ya huduma za kampuni ya teknolojia ya Google ikiwemo baruapepe ya Gmail hazipatikani mtandaoni, jambo ambalo limeibua usumbufu kwa watumiaji wa huduma hizo.

Huduma nyinginge ambazo baadhi ya watu wanalalamika kutozipata kuanzia mchana wa leo Desemba 14, 2020 ni mtandao wa YouTube, sehemu ya kuhifadhia nyaraka mtandaoni ya Google Drive na Google doc inayotumika kuandikia nyaraka mbalimbali.

Kwa kila anayetaka kufungua huduma hizo anakutana na ujumbe unaosema ” Samahani, akaunti yako haipatikani. Samahani kwa usumbufu uliotokea na jaribu tena baadaye.”

Mpaka sasa haijulikani ni changamoto gani imetokea kwa huduma hizo kutopatikana.

Pia watumiaji katika mataifa mengine wamelalamika kwa kukosa huduma hizo.


Soma zaidi:


Google imewaelekeza watumiaji wa huduma zake kutembelea kituo cha msaada cha kampuni hiyo yenye makao makuu nchini Marekani kwa ajili ya kupata taarifa zaidi.

Mtandao wa YouTube ni moja ya huduma maarufu ya Google inayowapatia fursa watumiaji wa mtandao kutazama na kusikiliza muziki na kupata habari za televisheni mtandao.

Pia, Google imekua ni kiungo muhimu kwa watu wanaofanyia kazi au biashara mtandaoni kwa sababu ni njia ya rahisi ya kuwasiliana na kutunza nyaraka.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
21 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: ULEGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI BUNGENI

🔴LIVE: ULEGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI BUNGENI

Nukta TV

NMB BANK YATANGAZA GAWIO LA SH610 KWA HISA 2025

NMB BANK YATANGAZA GAWIO LA SH610 KWA HISA 2025

Nukta TV

🔴LIVE: ULEGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI BUNGENI

🔴LIVE: ULEGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI BUNGENI

Nukta TV