Hii ndiyo hifadhi ya Taifa Rumanyika

February 3, 2020 1:46 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link

Kuona wanyama kama twiga, tembo, swala na hata ndege wa aina mbalimbali, Rumanyika itakukaribisha vilivyo mwezi Disemba hadi Februari. Picha| Pixabay.


  • Ina ukubwa wa kilometa za mraba 800
  • Milima na mabonde yake, ni kivutio cha nyani na wanyama wengine wengi.
  • Vipepeo, maua pori na ndege ni sehemu tu ya uzuri utakaokuvutia ukiitembelea

Dar es Salaam. Ni miongoni mwa hifadhi za Taifa mpya tano zilizoanzishwa mwaka 2019, ikiwa na vivutio vingi ambavyo ni fursa kwa watalii na kuiingizia Serikali mapato. Ni hifadhi ya Taifa ya Rumanyika. 

Endapo umezowea kuona Twiga na kusikia mtikisiko wa ardhi pale tembo anapotembea, hakika unahitaji kuitembelea hifadhi hii kwa ajili ya kubadilisha taswira yako ya kitalii kwani kati ya hifadhi za nchini, hifadhi ya Taifa ya Rumanyika itakupatia safari ya aina yake.

Siyo kwamba utashuhudia wanyama adimu tu kama ilivyo katika Hifadhi Taifa ya Mto Ugalla lakini Rumanyika inaenda mbali zaidi kwa kukupatia fursa ya kushuhudia sokwe na nyani wanavyoruka kutoka kwenye mti mmoja hadi mwingine.

Hifadhi ya Taifa ya Rumanyika ambayo ina ukubwa wa kilometa za mraba 800 ni hifadhi inayoipamba ardhi ya mkoa wa Kagera huku uzuri wake ukizidi kuwa wakipekee kwenye ardhi hiyo inayopakana na Ziwa Victoria.

Je, mara yako ya mwisho kuona vipepeo ni lini? Rumanyika itakupatia muda mzuri wa kuwashuhudia viumbe hao wanaofanya maua ya hifadhi hiyo kuzidi kuchanua kwenye kiwango cha joto kinachofikia Sentigredi 41.


Zinazohusiana


Unahisi imeishia hapo, ndege ambao husafiri kutoka maeneo mengine huipamba hifadhi hii kwa rangi huku miruzi wanayoitoa ikikusahaulisha “earphone” zako na muziki unaousikiliza.

Kuyaona hayo (maua pori na vipepeo) itakulazimu uitembelee hifadhi hii mwezi Juni hadi Agosti huku kama wewe unapendelea kuona wanyama kama twiga, tembo, swala na hata ndege wa aina mbalimbali, Rumanyika itakukaribisha vilivyo mwezi Disemba hadi Februari.

Hakika umepata sehemu kwa ajili ya kutalii mwishoni mwa mwaka ambayo inafikika kwa wepesi kwa barabara.

Kwa mujibu wa Tanzania Zalendo, Hifadhi hii inafikika kwa kutumia mabasi yanayotokea Kata ya Kaisho mkoani Kagera ambapo utasafiri umbali wa kilometa18.4 na kama utatokea Kaitambuzi (kagera), utasafiri umbali wa kilometa 27.1 hadi kuifikia hifadhi hiyo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV