HESLB yatangaza majina waliopata mikopo awamu ya kwanza 2025/26

October 24, 2025 3:09 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • 40,952 ni wa shahada ya kwanza na 5,342 wa stashahada ambao wamepangiwa mikopo yenye thamani ya Sh152 bilioni.

Dar es Salaam. Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa awamu ya kwanza ya upangaji mikopo na ruzuku kwa jumla ya wanafunzi 135,240 nchini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, leo Ijumaa, Oktoba 24, 2025, kati ya wanafunzi hao, 40,952 ni wa shahada ya kwanza na 5,342 wa stashahada ambao wamepangiwa mikopo yenye thamani ya Sh152 bilioni.

Aidha, wanafunzi 615 waliopo chini ya mpango wa Samia Scholarship wamepangiwa ruzuku yenye jumla ya Sh3.3 bilioni.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa wanafunzi 88,331 wanaoendelea na masomo wamepangiwa mikopo yenye thamani ya Sh271.2 bilioni baada ya kufaulu mitihani yao ya mwaka uliopita.

Bodi hiyo imebainisha kuwa itaendelea kutoa awamu nyingine za mikopo na ruzuku kadiri itakavyopokea uthibitisho wa udahili kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza na matokeo ya wanafunzi wanaoendelea.

HESLB pia imewakumbusha waombaji wa mikopo na ruzuku kuendelea kufuatilia taarifa za maombi yao kupitia mfumo wa Student’s Individual Permanent Account (SIPA) wakati taratibu za uchambuzi na upangaji zikiendelea.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: ULEGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI BUNGENI

🔴LIVE: ULEGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI BUNGENI

Nukta TV

🔴LIVE: HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA ULINZI NA IKISOMWA BUNGENI

🔴LIVE: HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA ULINZI NA IKISOMWA BUNGENI

Nukta TV

Fahamu kuhusu Virusi vya ‘Hantavirus’ na nini chanzo chake ?

Fahamu kuhusu Virusi vya ‘Hantavirus’ na nini chanzo chake ?

Nukta TV