Haya ndio maajabu ya iPhone Duo simu mpya kutoka Apple

September 12, 2026 10:17 am · Method Allen
Share
Tweet
Copy Link
  • Oda za awali za mauzo kuanza Oktoba 16, huku mauzo rasmi yakitarajiwa kuanza Oktoba 23, 2026.
  • Maajabu ya hii simu yapo kwenye kioo chake ambacho kina ukubwa wa inchi 5.4 ikiwa haijakunjuliwa na ukubwa wa inchi 7.6 ikiwa imekunjuliwa.

Dar es Salaam. Kila kona ya mitandao ya kijamii kwa sasa stori kubwa inayobamba ni kuhusu iPhone baada ya kampuni ya Apple kuzindua toleo jipya la Iphone 18 na iPhone Duo.

Hata hivyo, mjadala mkubwa kwa mwaka huu haupo kwenye series ya Iphone 18, bali kwenye iPhone Duo simu yenye kioo kinachokunjika iliyoingizwa kwa mara kwanza sokoni na kampuni hiyo.

Maajabu ya hii simu yapo kwenye kioo chake ambacho kina ukubwa wa inchi 5.4 ikiwa haijakunjuliwa na ukubwa wa inchi 7.6 ikiwa imekunjuliwa.

Kwa wale wapenzi wa kutazama movies, ‘animations’ au kucheza gemu hapa nafikiri Apple itakuwa imewakonga moyo.

Kwa upande wa chaji, iPhone duo inauwezo wa kuchaji ‘wireless’ yaani kuchaji bila kuchomeka waya, na ikiwa imejaa full, chaji yake inauwezo wa kudumu kwa saa 44 takriban siku 2 ikiwa utatumia skrini ndogo na ikiwa utatumia skrini kubwa chaji yake inaweza kudumu hadi saa 31 sawa siku moja na masaa saba.

Lakini pamoja na kukaa chaji kwa muda wote huu iPhone Duo inaweza kuingiza chaji kwa asilimia 50 ndani ya dakika 20 tu.

Kwa upande wa kamera, simu hii ina kamera mbili za nyuma ambapo kamera kuu inauwezo wa megapixel 48, na kamera ya mbele ikiwa na uwezo wa megapixel 12.

Tofauti na matoleo mengi mapya ya iPhone ulinzi wa iPhone Duo haujahusisha uwezo wa kufungua simu hii kwa kutumia FaceID na badala yake utaweza kufungua kwa fingerprint kupitia touch ID iliyowekwa pembeni ya kitufe cha kuwashia.

Kama ambavyo simu hii ni kali basi na bei yake pia imechangamka kidogo kwa sababu Apple imeweka bei ya kuanzia ya iPhone Duo kuwa Dola za Marekani 1,999, sawa na takribani Sh5.3 milioni ikiwa ni nje ya gharama za usafirishaji pamoja na kodi.

Kwahiyo mpaka simu hiyo inakufikia hapa bongo unaweza kuipata kwa gharama ya hadi Sh7 milioni au zaidi kutegemea na duka utakaloenda kununua.

Kwa bei hiyo, Duo inakuwa miongoni mwa simu zinazozalishwa na kampuni ya Apple zenye gharama kubwa zaidi, huku bei yake ikiwa juu ikilinganishwa na iPhone 18 Pro ambayo Apple waliizundua pia katika uzinduzi ulifanyika Septemba 9, 2026.

Hata hivyo, kelele zimekuwa nyingi sana kutoka kwa mtani wa jadi na  mshindani mkubwa wa kibiashara wa iPhone ambaye ni Samsung ambapo wengi wamedisi teknolojia hiyo wakisema kwamba hakuna kitu kipya kwani ilishatumika na kampuni nyingine kama vile Samsung na Huawei miaka mingi iliyopita.

Samsung ambaye ndiye mtengenezaji mkubwa wa vioo pamoja na kamera za simu za iPhone, ndiyo kampuni ya kwanza kutumia teknolojia ya vioo halisi vinavyokunjika miaka 6 iliyopita kupitia toleo lake la Galaxy Z Flip.

Apple imepanga kuanza kupokea oda za mauzo ya iPhone Duo kuanzia Oktoba 16, huku mauzo rasmi yakitarajiwa kuanza Oktoba 23, 2026.

Vipi, na wewe uko tayari kununua simu hiyo kwa zaidi ya milioni 5 au tukuache kwanza?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
12 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
12 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Haya ndio maajabu ya iPhone Duo simu mpya kutoka Apple

Haya ndio maajabu ya iPhone Duo simu mpya kutoka Apple

Nukta TV

Kitakachotokea IGP, CDF na DCI wasipofika mahakamani kesi ya Lissu

Kitakachotokea IGP, CDF na DCI wasipofika mahakamani kesi ya Lissu

Nukta TV

Jinsi waajiri wanavyokimbilia 'Interns' kukwepa ajira za kudumu

Jinsi waajiri wanavyokimbilia 'Interns' kukwepa ajira za kudumu

Nukta TV