Gavana Florens Luoga hajafungua akaunti Facebook-BoT

October 29, 2019 8:53 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Imesema Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Florens Luoga hajafungua akaunti ya Facebook, kinyume na taarifa na picha zinazojitokeza katika mtandao huo kwa jina lake.
  • Watanzania watakiwa kupuuza taarifa yoyote inayotolewa na akaunti hiyo bandia inayojiita Frolence Luoga.
  • BoT imeeleza kuwa hatua za kisheria zinaendelea kuchukuliwa ili kumbaini mhalifu aliyefungua akaunti hiyo.

Dar es Salaam. Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imesema Gavana wa benki hiyo, Profesa Florens Luoga hajafungua akaunti ya mtandao wa kijamii wa Facebook, kinyume na taarifa na picha zinazojitokeza katika mtandao huo kwa jina lake.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo (Oktoba 29,2019)  na Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki ya BoT imeutaka umma wa Watanzania kupuuza taarifa yoyote inayotolewa na akaunti hiyo bandia inayojiita Frolence Luoga na ambayo inatumia picha mbalimbali za Gavana wa BoT kinyume na sheria,

“Tunauhakikishia umma kwamba, Gavana Luoga hajafungua akaunti kwa jina hilo na hivyo taarifa zozote zitakazotolewa kwenye akaunti hiyo ya Facebook hazina uhusiano wowote na Prof. Florens Luoga,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo inayopatikana katika ukurasa wa Twitter wa BoT.

Hata hivyo, BoT imeeleza kuwa hatua za kisheria zinaendelea kuchukuliwa ili kumbaini mhalifu huyo kwa kutumia akaunti hiyo kuchafua sifa ya  Gavana Luoga kwenye jamii. 

Taarifa hiyo haijaeleza kwa undani ni kwa namna gani akaunti hiyo imechafua sifa ya Prof Luoga.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
14 Sep, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
14 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
14 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Haya ndio maajabu ya iPhone Duo simu mpya kutoka Apple

Haya ndio maajabu ya iPhone Duo simu mpya kutoka Apple

Nukta TV

Kitakachotokea IGP, CDF na DCI wasipofika mahakamani kesi ya Lissu

Kitakachotokea IGP, CDF na DCI wasipofika mahakamani kesi ya Lissu

Nukta TV

Jinsi waajiri wanavyokimbilia 'Interns' kukwepa ajira za kudumu

Jinsi waajiri wanavyokimbilia 'Interns' kukwepa ajira za kudumu

Nukta TV