Euro yaendelea kuimarika dhidi ya Shilingi ya Tanzania
- Ongezeko la thamani ya Euro linatokana na uhitaji mkubwa wa sarafu hiyo katika soko la fedha za kigeni
Dar es salaam. Sarafu ya nchi za Umoja wa Ulaya (Euro) imeendelea kuimarika dhidi ya Shilingi ya Tanzania, kwa mujibu wa takwimu za soko la ubadilishaji wa fedha zilizotolewa leo Julai 17, 2026
Takwimu zilizotolewa na benki za kibiashara za CRDB na NMB zinaonesha ongezeko la thamani ya Euro ikiwa ni tofauti na bei iliyotumika siku ya jana
Kupitia benki ya CRDB, Euro leo imenunuliwa kwa Sh2,864.44, kutoka Sh2,859.95 iliyonunulia jana sawa na ongezeko la Sh4.49
Bei ya kuuza nayo imepaa kwa Sh7.49 kutoka Sh3,156.95 iliyotumika jana hadi Sh3,164.44 inayotumika leo.
Kwa upande wa Benki ya NMB, Euro leo imenunuliwa kwa Sh2,880, kutoka Sh2,872 ya jana, na bei ya kuuza nayo imepanda kutoka Sh3,145 hadi Sh3,152.
Ongezeko la thamani ya Euro linatokana na uhitaji mkubwa wa sarafu hiyo katika soko la fedha za kigeni, hali inayopelekea wafanyabiashara wanaotumia Euro katika miamala yao ya kila siku kunufaika zaidi kwa kupata shilingi nyingi na kuingiza mpunga wa kutosha.
