Bei ya mahindi yashuka Dodoma

May 22, 2020 1:37 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei ya juu ya zao hilo kwa kilo 100 mkoani humo imeshuka hadi Sh45,000 kutoka Sh59,000 Ijumaa iliyopita.
  • Lindi ndiyo mkoa ambao mahindi leo yanauzwa kwa bei ya juu zaidi Tanzania.

Dar es Salaam. Bei ya jumla ya mahindi katika Mkoa wa Dodoma imeshuka kwa takriban asilimia 23.7 ndani ya kipindi cha wiki moja, jambo linawapa ahueni wanunuzi wa zao hilo katika mkoa huo uliopo katikati mwa Tanzania. 

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa leo (Mei 22, 2020) na Wizara ya Viwanda na Biashara zinaonyesha kuwa bei ya juu ya gunia la kilo 100 la zao hilo linauzwa kwa Sh45,000 katika soko la Majengo mkoani humo.

Hata hivyo, bei hiyo ya juu imeshuka kwa asilimia 23.7 kutoka Sh59,000 iliyorekodiwa Ijumaa Mei 15, 2020 mkoani humo katika soko hilo hilo. 

Katika takwimu za leo, bei ya chini ya zao hilo katika soko hilo la Majengo imeporomoka hadi Sh40,000 kutoka Sh48,000 iliyorekodiwa wiki iliyopita.    

Kushuka kwa bei hiyo ya juu kutawanufaisha zaidi wanunuzi huku wafanyabiashara na wakulima wakipoteza wastani wa Sh14,000 kwa kila gunia moja iwapo hesabu hizo zitapigwa kwa viwango vya bei ya juu. 

 Aidha, takwimu hizo zinaonyesha kuwa bei ya juu ya zao hilo la chakula inayotumika leo ni Sh115,000 katika Mkoa wa Lindi huku bei ya chini ikiwa ni Sh32,000 katika Mkoa wa Ruvuma. 

Endelea kusoma www.nukta.co.tz kwa kwa habari zaidi za takwimu kuhusu bei za mazao, soko la hisa na nyingine za biashara. Kwa habari zaidi Whatsapp +255 677 088 088 au newsroom@nukta.co.tz

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.