Bei ya mahindi yashuka Dodoma

May 22, 2020 1:37 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei ya juu ya zao hilo kwa kilo 100 mkoani humo imeshuka hadi Sh45,000 kutoka Sh59,000 Ijumaa iliyopita.
  • Lindi ndiyo mkoa ambao mahindi leo yanauzwa kwa bei ya juu zaidi Tanzania.

Dar es Salaam. Bei ya jumla ya mahindi katika Mkoa wa Dodoma imeshuka kwa takriban asilimia 23.7 ndani ya kipindi cha wiki moja, jambo linawapa ahueni wanunuzi wa zao hilo katika mkoa huo uliopo katikati mwa Tanzania. 

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa leo (Mei 22, 2020) na Wizara ya Viwanda na Biashara zinaonyesha kuwa bei ya juu ya gunia la kilo 100 la zao hilo linauzwa kwa Sh45,000 katika soko la Majengo mkoani humo.

Hata hivyo, bei hiyo ya juu imeshuka kwa asilimia 23.7 kutoka Sh59,000 iliyorekodiwa Ijumaa Mei 15, 2020 mkoani humo katika soko hilo hilo. 

Katika takwimu za leo, bei ya chini ya zao hilo katika soko hilo la Majengo imeporomoka hadi Sh40,000 kutoka Sh48,000 iliyorekodiwa wiki iliyopita.    

Kushuka kwa bei hiyo ya juu kutawanufaisha zaidi wanunuzi huku wafanyabiashara na wakulima wakipoteza wastani wa Sh14,000 kwa kila gunia moja iwapo hesabu hizo zitapigwa kwa viwango vya bei ya juu. 

 Aidha, takwimu hizo zinaonyesha kuwa bei ya juu ya zao hilo la chakula inayotumika leo ni Sh115,000 katika Mkoa wa Lindi huku bei ya chini ikiwa ni Sh32,000 katika Mkoa wa Ruvuma. 

Endelea kusoma www.nukta.co.tz kwa kwa habari zaidi za takwimu kuhusu bei za mazao, soko la hisa na nyingine za biashara. Kwa habari zaidi Whatsapp +255 677 088 088 au newsroom@nukta.co.tz

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV