Bei ya mahindi yaleta tofauti Lindi, Mara

March 18, 2020 11:37 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Gunia la kilo 100 la mahindi linauzwa kwa Sh120,000 katika Mkoa wa Lindi wakati Mara linauzwa Sh45,000.
  • Wafanyabiashara wa Lindi huenda wakafaidika maradufu kuliko wale wa Mara.

Huenda wafanyabiashara wa mahindi katika Mkoa wa Lindi leo wataneemeka kwa mauzo mazuri baada ya mkoa huo kurekodi bei ya juu ya zao hilo ikilinganishwa na maeneo mengine nchini Tanzania.

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa na Wizara ya Viwanda na Biashara leo (Machi 18, 2020) zinaonyesha kuwa gunia la kilo 100 la mahindi linauzwa kwa Sh120,000 katika Mkoa wa Lindi. 

Bei hiyo inayotumika katika masoko ya mkoa huo ndiyo bei ya juu kabisa nchini Tanzania, jambo linalowafaidisha wafanyabiashara waliopeleka zao hilo katika mkoa huo wa kusini mwa Tanzania. 

Hata hivyo, wenzao wa Musoma mkoani Mara guni hilo hilo la kilo 100 wanauza kwa Sh45,000 ikiwa ni pungufu zaidi ya mara mbili ya bei inayotumika Lindi. 

Bei hiyo inayotumika Mara ndiyo bei ya chini kabisa ikilinganishwa na maeneo mengine nchini.

Mahindi ni zao linalotegemewa na kaya nyingi nchini kwa chakula.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW