Kicheko, maumivu bei ya mahindi ikipanda

April 21, 2023 6:54 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Imepanda kwa asilimia 84.1  ndani ya kipindi cha mwaka mmoja unaoishia Februari 2023.

Dar es Salaam. Huenda Watanzania wakaendelea kutoboa mifuko yao zaidi baada ya bei ya mahindi kupanda kwa asilimia 84.1  ndani ya kipindi cha mwaka mmoja unaoishia Februari 2023.

Mahindi ni sehemu ya mazao makuu ya chakula yanayotumiwa kwa wingi na Watanzania. Mazao mengine ni maharage, mtama, uwele na viazi.

Ripoti ya Tathmini ya Uchumi ya Machi 2023 (Monthly Economic Review) iliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) hivi karibuni imeeleza kuwa bei ya jumla ya gunia la kilo 100 la mahindi kwa mwaka ulioishia Februari 2023 ilikuwa inauzwa kwa Sh114,762 kutoka Sh62,326 ya kipindi kama hicho mwaka 2022. 

Hilo ni sawa na ongezeko la Sh52,436 au na asilimia 84.1.

​Ni kawaida katika kama hiki ambacho wakulima wanaendelea kuotesha mazao shambani, bei kupanda kwa sababu bidhaa za vyakula zinakuwa hazipatikani kwa wingi sokoni.

Kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo kunawaumiza walaji kwa sababu wanalazimika kutoboa zaidi mifuko yao zaidi ili kupata zao hilo la chakula, wakati wakulima wananeemeka na bei hiyo.

Hata wakati bei ya mahindi ikipaa kwa asilimia 84.1 zaidi ya ile ya mwaka 2021, bei hiyo imekuwa ikipanda na kushuka tangu Machi mwaka jana. Mathalan, Januari mwaka huu bei ya mahindi ilikuwa Sh115,852 na mwezi uliofuata imeshuka hadi Sh114,762.  

Siyo tu mahindi, karibu bei za mazao yote ya chakula zimepanda ndani ya mwaka mmoja uliopita. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
6 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
6 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV